Tuesday, 24 September 2013

         MESHACK ABEL MWAMKINA
                                   IMEANDIKWA NA ABDUL SUDI,MBEYA

        
                                                    meshack abel akimdhibiti mshambuliaji wa Gor Mahia    Alizaliwa Mbeya,eneo la Ghana na kusoma katika shule ya msingi Mbata na baadae sekondari akasoma Sangu.
    Kama ilivyo kwa watoto wengi wa Tanzania Meshack Abel alianza kucheza mpira toka akiwa mdogo sana,kwanza jirani na kwao,kisha kidogo kidogo kipaji chake kilipoanza kuonekana akawa anachukuliwa na wenzake na kwenda kucheza mbali kidogo na nyumbani kwao.huko alikutana na watoto wengi wenye vipaji kama vyake na ikawa rahisi kumshawishi na kwenda kuingia katika ligi za watoto zilizokua zikifanyika katika sehemu iliyojulikana kama kiwanja ngoma,kwake ilikua ni rahisi kwani kaka yake aliyekua akiitwa Reuben au maarufu kama ‘masox’alikua ndie mchezaji maarufu zaidi ya watoto wengi wa eneo lile,hivyo alikua kama kamsafishia njia,lakini Meshack hakumuangusha kaka yake kwani nae akatokea kua mzuri zaidi ya  kaka yake.
    Hapo Kiwanja ngoma aliichezea kwanza timu iliyoitwa Saitama na baadae Snow White na alikutana na watoto wengi waliokua na viwango vya juu sana na ambao karibu wote baadae walikuja kucheza katika ligi kuu ya Tanzania.Mbali na kaka yake Reuben aliekuja chezea AFC ya Arusha,alikutana na kina Jaafar Muhoza,Vicent Barnabas,Yona Ndabila,Shaaban Mtupa,Mbega Daffa,Misengo Magai,David Naftari,Bantu Admin,na wengine wengi.wakati huo alikua akicheza nafasi ya kiungo,ambayo mwenyewe anasema alikua anaimudu sana.
    Meshack alitoka moja kwa moja kiwanja ngoma na kuchukuliwa na timu ya AFC iliyokua ikicheza ligi kuu ya Tanzania,na huko alicheza katika kiwango cha juu sana kiasi kocha aliyekua akiifundisha Mtibwa wakati huo Sunday Kayuni alimchukua na kumuhamishia katika timu ya Mtibwa,na ni yeye Sunday Kayuni aliyembadilisha namba kutoka kiungo na kumrudisha nyuma namba ambayo anacheza hadi leo.Baada ya kucheza Mtibwa kwa mafanikio viongozi wa Simba wakamfuata na kumtaka ajiunge na timu yao,ndipo alipojiunga na Simba,Alipokua Simba alichaguliwa na Maximo katika timu ya taifa.alikaa Simba kwa muda kisha akahamia Kenya katika timu ya Bandari ambayo ndio yupo hadi sasa.

            MESHACK ABEL (WA PILI KULIA)AKIWA NA KIKOSI CHA BANDARI YA KENYA      
Nilipomuuliza tofauti ya mpira wa Tanzania na Kenya akanambia “Unajua wenzetu huku wanajali sana kazi zao,huwezi kukuta mchezaji anachelewa mazoezini bila sababu maalum,na pia wachezaji wa huku wanamsikiliza sana kocha tofat na kwetu wachezaji wanakua juu ya kocha,na hata upangaji wa timu huku anaachiwa kocha moja kwa moja lakini Tanzania kocha anakua chini ya viongozi na wao ndio wanapanga timu na kujidai kama wanamshauri kocha,kumbe wanamlazimisha wanachotaka,mfano timu kama Simba ina bahati sana ya kupata makocha wazuri mno wa kiwango cha juu,lakini wanaingiliwa na viongozi na wafadhili hadi wanachanganyikiwa,mimi binafsi ukiniuliza kocha niliyekua namkubali sana Simba na ikaniuma sana aliopoondoka nitakwambia ni Benziski,Yule jamaa alikua anajua sana niliumia sana alipoondoka”aliongeza Meshack ambae anakiri kuwa kwake kama mtanzania yeyote mechi kubwa sana alizowahi kucheza hapa Tanzania ni kati ya Simba walipocheza na Yanga “mechi ya Simba na Yanga ndio mechi yangu kubwa hadi sasa kuicheza kwani ingawa inakua ni ya dakika 90 lakini inachukua muda mrefu sana kuzungumziwa na utayarishwa kiasi mnakua mnaisubiri kwa hamu sana….”alinambia Meshack