Tuesday, 20 August 2013

  “   THE TALENTED”
Uhuru selemani
  imeandikwa na Abdul "be good"Sudi/picha kwa hisani ya uhuru selemani.



       Mmoja kati ya wachezaji wenye vipaji halisi hapa Tanzania ni Uhuru Selemani,kwani pamoja na misuko suko ya majeruhi iliyokua ikimkabili lakini kila akiingia uwanjani anaonyesha kiwango kile kile alichokua nacho kabla ya kuumia.Na sasa hivi ,yupo vizuri  zaidi ya alivyokua misimu iliyopita. “namshukuru Mungu sasa hivi nipo salama,sina tatizo tena na naomba uzima nitaonyesha kiwango kikubwa zaidi ya nilichoonyesha kabla”alinambia Uhuru ambae kwa sasa yupo Coastal Union akitokea klabu ya SImba aliyokua nayo msimu uliopita. “unajua ukiwa majeruhi wa mara kwa mara hata wewe mwenyewe unachanganyikiwa,unakua hujiamini,uoga wa kuumia unakufanya usicheze kwa uhuru unaoutaka,lakini kwa sasa niko vizuri mno na naamini nitaonyesha kiwango changu halisi”
         Uhuru ana uwezo wa kucheza namba nyingi uwanjani,kwani pamoja na mara kwa mara kuchezeshwa kama kiungo wa pembeni lakini ana uwezo wa kusimama kama mshambuliaji na hata  kucheza kama kiungo wa juu.na kama lilivyo jina lake yupo huru sana akiwa na mpira kiasi ana uwezo wa kupiga chenga huku anakwenda mbele na pia ana uwezo wa kupiga miguu yote hivyo inakua ni ngmu sana kwa mabeki kumkaba akiwa na mpira,wanakuwa hawajui ataufanya nini mpira,na hata ukitazama magoli anayofunga ni ya uhakika si ya kubahatisha,kwa vile ana kipaji halisi.ni wachezaji wachache sana wenye uwezo wa kkupiga mashuti huku wanakimbia,lakini Uhuru anafanya hivyo mara kwa mara…

    Uhuru Selemani alizaliwa mkoani Mbeya katika wilaya ya Mbarali na alianza elimu yake ya awali katika shule ya  msingi Mbarali na kuja kumalizia Kawe Dar es salaam “toka nikiwa shule ya msingi nilipenda kucheza mpira,kiasi nilipokua mkubwa kidogo nikajiunga na wenzangu katika timu ya Ibara kids,pale tumecheza sana kisha baadae nikachukuliwa na rujewa kids zote za Mbeya na hata nilipohamia Dar moja kwa moja nikajiunga na ukwamani kids yak awe,,na huko tukawa tunafanya vitu vikubwa kiasi tukapata mashabiki wengi sana….unajua nimecheza mashindano ya muungano Mufindi nikiwa na umri mdogo sana lakini nilikubalika kwa vile kiwango changu kilikua ni cha uhakika”
     Uhuru amewahi kuchezea timu kadhaa ikiwemo Mtibwa,Coast,Azama ,na Simba  ana uzoefu wa kucheza katika hali  yoyote “Ninashukuru nimeanza kucheza mpira wa ushindani nikiwa mdogo sana hilo limenikomaza na kuweza kupambana na changamoto za kila aina,kila timu unayokwenda unakuta ina mifumo yake,tokay a uchezaji hadi ufundishaji,hivyo nimepitia mambo mengi sana sasa hvi nishakua mzoefu wa fitna za soka”alinielezea. “Nafurahia sana maisha ndani ya timu yangu ya Coastal Union,kwani hakuna mazengwe ya kutengenezeana,hapa mtu unacheza kutokana na kiwango chako,tofauti na inavyokua kwa timu hizo zinazoonekana ni kongwe hapa Tanzania,kule mwenye sauti ya mwisho nani acheze na nani asicheze si kocha,ni watu tofauti kabisa wenye nguvu za ajabu katika hizo timu,ndio maana utashangaa kila siku wanaacha wachezaji wazuri na kusajili vichekesho,nimepita huko najua naloongea,unafanya mazoezi vizuri,kocha anakufurahia na kukusifu na kukupa matumaini unajua mechi inayokuja unacheza lakini baadae ikitajwa list unakua haupo,kisha unaanza kusikia rumours,kua kuna kiongozi pengine hakupendi au hataki ucheze…unaweza hata kuzushiwa sababu za ajabu…huna nidhamu au lolote na itokee bahati mbaya ukakosea siku uliyopangwa mashabiki wale wale wa timu yako ndio wanakua wa kwanza kukupigia kelele na kumlazimisha kocha akubadili…siwalaumu kwani najua wanakua tayari wameshalishwa sumu”aliongea Uhuru “lakini kwa timu nyingine hali ni tofauti,presha inakua ndogo ndio maana hata mchezaji unakua na amani na unafanya vizuri.

     Uhuru amechaguliwa mara kadhaa kuichezea timu ya Taifa,na mechi ambayo kila mtu anaikumbuka ni siku Tanzania walipocheza na Brazil “kila mtu duniani anatamani kucheza na Brazil,nashukuru mumngu nilipata nafasi ya kucheza na wachezaji bora kabisa duniani,mara nyingi unawaona katika tv lakini nimebahatika kucheza nao…fikiria unacheza na mchezaji unaempenda kama Robinho,unakabwa na mchezaji kama Dani Alves,hiyo ni kumbukumbu nitakayobaki nayo hadi nakufa maana si wote wenye bahati kama yangu”

   Kwa sasa Uhuru amesajiliwa na timu ya Coastal Union ya Tanga akitokea timu ya Simba.na kwa matayarisho aliyoyafanya ana uhakika wa kucheza vizuri zaidi  msimu huu….tuko pamoja HOME BOY……

Sunday, 18 August 2013

               David Mwantika
       "HOME BOY"
                                 IMEANDIKWA NA ABDUL"be good"SUDI,MBEYA.
                                       PICHA KWA HISANI YA DAVID MWANTIKA


                                                              DAVID MWANTIKA
         
Sifa kubwa ya beki ni kutumia nguvu na akili,kucheza mipira ya juu na kuusoma mchezo.hivyo vyote  anavyo David Mwantika,ambae uhodari wake wa kutumia nguvu na akili umemfanya awe mmoja kati ya mabeki wazuri sana hapa Tanzania,ana uwezo wa kupiga miguu yote miwili,anajua sana kukaba,iwe man to man au hata kukaba nafasi,pia ni mzuri sana wa kutazama mashambulizi kabla hayajafika hivyo mara nyingi amekua akiwapanga wachezaji wenzake ili kuziba njia zote na kulifanya lango lao liwe salama.na kikubwa anachowazidi mabeki wengine ni kua ni mzuri sana kucheza mipira ya juu,hivyo ana uhakika wa asilimia nyingi wa kumlinda kipa wake.

                                   MWANTIKA AKIMDHIBITI SAID BAHANUZI  WA YANGA
      “Kucheza mpira si nguvu peke yake,na akili ina nafasi yake,hivyo kikubwa kinachotakiwa unapokua uwanjani ni kuwa makini muda wote wa mchezo,usiondoe mawazo mchezoni hata kwa sekunde moja kwani unapojisahau hapo hapo watu wanatumia nafasi na kuwaumiza”alinambia nilipoongea nae. “mifano ipo mingi,mnaweza kua mnacheza na kujiona kama tayari mmewazidi mmnaocheza nao,mnajiamini na hapo ndio kosa kubwa linapofanyika kwani nao wanakua wanajipanga wapate nafasi,mkikosea kidogo wanawapiga bao inakua kazi kuanza kutafuta la kurudisha”Alinifafanulia Mwantika aliyezaliwa mkoani Mbeya sehemu inayoitwa Ilomba,mbele kidogo ya kitongoji maarufu sana cha MWANJELWA ambacho kina pilika pilika nyingi mno za biashara.Alisoma elimu ya awali katika shule ya msingi Ilomba,ambapo ndipo alipoanzia kucheza soka “pale shuleni kulikua na ushindani sana wa soka,maana kama kukiwa hakuna kipindi kinachofanyika ni kuchukua mpira na kwenda kiwanjani,na huko ilikua ni mashindano maana timu mbili ndio zinashindana kila siku,na hakuna inayookubali kushindwa”alinieleza David ambae toka akiwa darasa la nne alikua akiichezea timu ya shule “nimecheza sana mashindano ya umitashumta,na wakati nipo shule nikawa nachukuliwa na timu moja ya mtaani ikijulikana kama  HOME BOYS na huko nilkutana na washikaji wengi sana wanaojua soka la nguvu,nikawa napambana kupata namba na pale ilinisaidia sana kwani nilianza kujifunza kuwa nikicheza vibaya sipangwi,nikawa najituma sana kufanya mazoezi na nikipata nafasi ya kucheza mechi nafanya kweli”aliniambia huku akitabasamu baada ya kuwakumbuka rafiki zake aliokua nao HOME BOYS…. “kulikua na mafundi sana pale HOME BOYS bahati mbaya hawakupata nafasi ya kucheza timu kubwa kwani nawakumbuka rafiki zangu kina GWAKISA,AMULIKE na hata mdogo wangu aliyeitwa ATU walikua wanajua sana mpira,ni mazingira mabovu ndio yamesababisha hadi wakapotea”aliongeza kwa masikitiko.
       Wakati akiwa HOME BOYS viongozi wa timu ya kijiweni ya Uyole Mbeya wakamuona na kumchukua. “KIJWENI nako niliikuta timu ina ushindani sana,lakini nilipigana hadi nikawa na namba ya kudumu,tukacheza ligi daraja la kwanza ingawa hatukufanikiwa kupanda lakini ilikua ni timu bora sana nako kulikua na mafundi ambao kila siku nazidi kushangaa kwa nini hawakuja kucheza ligi kubwa,mtu kama EZE,MTUMBA na hata MOI walikuwa wanajua sana soka tofauti na watu wengi naokutana nao huku wanachezea timu kubwa huku viwango vyao ni vya kawaida sana,lakini ndio maisha,kila mtu na alichopangiwa”akasisitiza.


                                 DAVID MWANTIKA AKIMZUIA FELIX  SUNZU  WA SIMBA 
         Alipotoka KIJIWENI akachukuliwa na timu ya POLISI Mbeya ambako hakukaa sana akaenda  PRISON ya Mbeya ikiwa katika ligi kuu ya Tanzania bara,na huko alifanya sana kazi na kufanikiwa kua na namba ya kudumu. “kule PRISON timu ilikua nzuri na tulikua tunafanya sana mazoezi hivyo tulikua tupo fit sana,tatizo kubwa mechi za nyUmbani zilikua zinatusumbua kutokana na mashabiki kugawanyika kila tunapocheza,inakua kama unacheza ugenini,hadi leo sijui sababu gani watu walikuwa hawataki tushinde wakati nao ni watu wa Mbeya,siwezi kuwasemea kwani wao wanajua sana sababu zao”
        Baada ya kucheza kwa misimu kadhaa ndipo alipochukuliwa na AZAM mbako yupo hadi sasa. “hapa  AZAM timu imetulia,tuko vizuri sana,hata ikitokea mechi tumepoteza tunajua ni bahati mbaya lakini kwa vipaji na uwezo tupo juu ya timu zote za Tanzania,msimu huu unaoanza tuna uhakika wa kufanya vizuri zaidi ya misimu iliyopita,labda yaanze tena mazengwe ya vilabu vinavyojiita vikubwa lakini kwa soka tu tuko vizuri mno”alinambia Mwantika ambae katika mechi ya kombe la shirikisho dhidi ya timu ya AFR ya Morocco alitolewa kwa kadi nyekundu kwa mazingira ya ajabu sana. “hadi leo nikitazama tape za ile mechi namshangaa refa kwa nini alinitoa nje maana ile ilikua ni shoulder to shoulder,nikamzidi nguvu,lakini ajabu nashangaa nikapewa kadi nyekundu,niliumia sana kwani pale ndipo mechi ilipoishia,maana kabla ya kadi nyekundu tulikua tumeshawashika……”alinambia Mwantika.


                                 DAVID MWANTIKA AKIMTOA NJIANI MRISHO NGASA
       David amepania sana kujituma kwa bidii zaidi ili waweze kutimiza lengo lao na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Tanzania. “kwa jinsi timu yetu ilivyo nzur sasa hivi,na ukichukulia tumeshakaa muda mrefu pamoja hatuna sababu ya kutufanya tushindwe kuchukua ubingwa”alisema Mwantika anaemkubali sana mshambuliaji wa timu yake  Gaudence Mwaikimba.”tutapigana hadi dakika ya mwisho najua tutashinda”alimalizia …Huyu ndio David Mwantika……HOME BOY  aliyepigana kutoka Ilomba Mwanjelwa Mbeya hadi AZAM FC,na bado safari inaendelea....……