Thursday, 6 March 2014

yanga na ahly kucheza Alexandria

    Mchezo wa marudiano kati ya Yanga na Al Ahly ya Misri umepangwa kufanyika katika uwanja wa  Harras el Hadoud uliopo Alexandria Misri  siku ya jumapili, badala ya jijini Cairo.
Taifa stars sare na Namibia

Timu ya soka ya Taifa Stars ya Tanzania, wametoka sare na Brave Warriors ya Namibia kwa kufungana goli moja kwa moja katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.

Monday, 3 March 2014

Kocha mwambusi
BADO TUPO VIZURI

Kocha mkuu wa timu ya Mbeya City, Juma mwambusi amesema timu yake bado iko vizuri pamoja na matokeo waliyopata karibuni.
     Timu hiyo imetoka sare na JKT Oljoro katika mchezo wake wa mwisho, na kabla ya hapo ilipoteza kwa timu ya Coastal Union ya Tanga.

Sunday, 2 March 2014

Simba yazinduka

Simba imezinduka baada ya kuifunga  Ruvu Shooting kwa magoli  3-2, katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara. Hadi mapumiko Simba walikua wakiongoza kwa magoli mawili yote yakifungwa na Amis Tambwe.