Friday, 11 October 2013

TZ PRISON KUWAVAA SIMBA

                                                                                      TZ PRISON
Timu ya TZ Prison ya mbeya jumamosi inakutana na Simba katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.Katika mchezo huo Tz Prison wataingia huku wakiwa tayari na kumbukumbu ya kuwafunga timu ya  Mgambo shooting katka mechi yao ya mwisho huku Simba wakitoka sare na timu ya Ruvu shooting.Mechi hiyo inatarajiwa kua ngumu kwani timu ya Tz Prison katika mechi za karibuni imeonyesha kiwango kizuri tofauti na ilipokanza ligi,wakati Simba kila siku kiwango kinazidi kushuka hivyo kwa kiasi kikubwa Tz  Prison wanajiamini na wana uhakika wa kupata point zote tatu.Katika mechi tatu za mwisho timu ya Tz prison ilitoka sare mbili na Azam na Mtibwa kabla hawajawafunga Mgambo 1-0,wakat Simba ilitoka sare ya 2-2 na Mbeya City kisha ikaifunga Ruvu JKT 2-0 kabla haijatoka sare tena na Ruvu shooting kwa goli 1-1.Lakini imekua ikilalamikiwa sana na mashabiki wake kutokana na kiwango cha chini inachokionyesha pamoja na kushinda.,Mechi nyingine itakayochezwa kesho itawakutanisha Kagera Sugar na Yanga mjini Kagera.

                                KILA LA HERI TZ PRISON

Wednesday, 9 October 2013

AMSHA AMSHA MBEYA CITY……
Waichapa Rhino 3-1


Timu ya Mbeya City imefanikiwa kupata ushindi mzuri ugenini baada ya kuifunga timu ngumu ya Rhino ya Tabora magoli matatu kwa moja katika mchezo wa ligi kuu ya Vodacom  uliochezwa katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mkoani Tabora.Katika mchezo huo Mbeya City walianza kwa kasi na kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa Rhino lakini umahiri wa golikipa wa Rhino uliwazuia washambuliaji wa Mbeya City kupata magoli mengi.magoli ya mbeya City yalifungwa na Jeremiah Juma,Alex Setth na la tatu likafungwa na Peter Mapunda. Na katika mchezo mwingine wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania Azam wamefanikiwa kuifunga Mgambo Shooting kwa magoli  2-0, magoli ya Azam yalifungwa na mchezaji aliyepandishwa katika kikosi hicho Farid Maliki katika dakika ya 67 kufuata pasi nzuri aliyopewa na  Erasto Nyoni,na goli la pili lillifungwa na  Kipre Tcheche kwa njia ya penati baada ya mshambulia ji wa Azam Farid kuangushwa ndani ya kumi na nane.Nayo timu ya Mtibwa imewafunga Ruvu JKT kwa magoli 2-1,kwa magoli ya haraka haraka yaliyofungwa na Juma Luzio dakika ya 3 ya mchezo baada ya kazi nzuri ya mkongwe Shaaban Kisiga kuwapunguza mabeki wa JKT na kumpa pasi mfungaji,goli la pili lilipatikana dakika mbili baadae baada ya Mtibwa kufanya shambulizi kali langoni mwa JKT na Juma Luzio akafunga baada ya kupata pasi toka kwa Abdallah Juma.goli la JKT lilifungwa na Salum Machaku baada ya kupiga kona iliyokwenda moja kwa moja wavuni. Nayo JKT oljoro imetoka sare ya magoli 2-2 dhidi ya Ruvu Shooting.    
MBEYA CITY KUCHEZA NA RHINO

                                                                                                MBEYA CITY FC
Timu ya Mbeya City leo inacheza na timu ya Rhino ya Tabora katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.Akiongea na Mbeya Maskan kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi amesema timu katika hali nzuri,na wanatarajia mchezo utakua mgumu na mzuri kwani wanaiheshimu Rhino kwa jinsi wanavyocheza lakini wamejitayarisha vizuri kukabiliana nao,na mungu akipenda atashnda.Hadi sasa Mbeya City imecheza mechi tatu ugenini,dhidi ya Mtibwa wakatoka sare ya 0-0,kisha wakacheza na Simba pia wakatoa sare ya 2-2 kabla hawajacheza na Oljoro na kuifunga 1-0.Mbeya City wamepania kushambulia sana katika mchezo wa leo,kwani wanahitaji point tatu ili wazidi kusogea juu zaidi katika msmamo wa ligi kuu.Mbeya City wanashika nafasi ya 11 wakiwa na point 11,wakishinda leo watapishana kwa pointi moja na kinara wa ligi hiyo Simba wenye pointi 15.
KIKOSI CHA MBEYA CITY LEO KITAKUA
1.David Baruan
2.John Kabanda
3.Hassan Mwasapile
4.Deo Julius
5.Anthony Mayunga
6.Yusuph Abdallah
7.Alex Setth
8.Steven Mazanda
9.Paul Nonga
10.Jeremiah John
11Deus Kaseke.

KILA LA KHERI MBEYA CITY.

Tuesday, 8 October 2013

ADNAN JANUZAJ
KINDA LA MAN UTD

Adnan Januzaj  amecheza mechi moja tu kamili toka ajiunge na timu ya Manchester United,lakini nchi tano zote zinataka akachezee timu zao za taifa.Nchi za Uturuki,Serbia,Kosovo na Albania pamoja na nchi aliyozaliwa ya Ubelgiji zote zinataka azichezee,na hata Uingereza nao wameanza  kampeni za chini chini za kutaka kumchukua ili awe raia wa nchi yao.
Januzaj alizaliwa Ubelgiji,ingawa wazazi wake walitokea Albania,ingawa nao kwao ni Kosovo.na walikuwa wamekimbia vita hivyo wakapata uraia wa Ubelgiji.
Alichukuliwa na timu ya Anderlecht ya ubelgiji alipokua na miaka 10 na akakaa hapo hadi alipofikisha miaka 16 ndipo akachukuliwa na Manchester United.Wakati kocha wa zamani wa Manchester United anataka kujiuzulu alimkabidhi Januza jezi namba 44.Mechi yake ya kwanza ilikua ni katika kombe la ngao ya hisani dhidi ya Wigan alipoingia badala ya Van Persie,nay a pili alimbadili Ashley Young walipocheza na  Crystal Palace,na mechi ya tatu ambayo alianza toka mwanzo ni walipocheza na Sunderland na akafanikiwa kufunga magoli yote mawili waliposhinda 2-1.

Ni mchezaji mwenye kasi,anaetumia sana mguu wa kushoto,anapiga chenga na anajua kufunga.alifanya vizuri sana wakati wa michezo ya majaribio kabla ya kuanza kwa msimu huu,na ingawa bado ana umri mdogo wa miaka 18 tayari kishaonyesha atakua ni mmoja kati ya wachezaji wazuri sana duniani.
 Ingawa nchi zote hizo zinataka akachezee timu zao za taifa lakini mwenyewe bado hajaamua akacheze wapi,lakini baba yake anasema atafurahia sana kama akiichezea nchi ya Albania.

Monday, 7 October 2013

MASHABIKI WA MBEYA CITY WALIVYOSUMBUA ARUSHA
                                                                                                  NA ABDUL SUDI.

                                                 
Kundi la mashabiki wa timu ya Mbeya City walisafiri kuifata timu yao ilipokwenda Arusha kupambana na JKT Oljoro,Baada ya kufika Arusha walikutana na wennzao waliokua wanaishi pale pale na kuanza kusherehekea kabla hata mechi haijaanza.wakizungumza na  Mbeya Maskan’ wamesema wameamua kwa mapenzi yao kwenda mji wowote timu itakapokua ikicheza ili kuipa sapoti na kuona wenyewe kwa macho yao  timu wanayoipenda ikicheza.Mmoja wa mashabiki hao Ally Makenya “popo”ambae ndie aliyeshughulika na kuwapokea mjini hapo alisema wanapata faraja sana kuona timu ya nyumbani inafanya vizuri na haibahatishi hivyo wapo tayari kwa hali na mali kuhakikisha inapata sapoti kubwa nje ya uwanja na wao wapo tayari kutoa sapoti hiyo.
ALLY MAKENYA AKIHAMASISHA

Muda wote wa mchezo walikua wakishangilia na kuwafanya wakazi wa Arusha kuwashangaa wanatoa wapi nguvu hiyo ya kushangilia.akiongelea hilo mkazi wa Arusha Josef Malya alisema amezoea kwenda kutazama mechi nyingi sana hapo arusha hata zikija timu kubwa za Yanga na Simba lakini hajawahi kuona  watu wanaoshangilia kwa moyo kama hawa mashabiki wa Mbeya City “hawa jamaa wanshangilia hata kama wanafanya vibaya tofauti na mashabiki wa Yanga na Simba ambao mchezaji wao akikosea wanamzomea lakini hawa wanashangilia tu na kuwapa moyo wachezaji wao,inafurahisha sana”alimalizia Malya.mtu mwingine aliyekuwepo uwanjani ni mfanyabiashara kutoka Shinyanga Abraham Shija,yeye anasema hajawahi kuona watu wanafurahia timu yao kama mashabiki wa Mbeya City,kwani toka mchana kabla kabisa ya mchezo haujaanza tayari walikua wameiteka mitaa ya Arusha na kuonekana kama burudani mpya mjini hapo “nasikia jamaa wamesafiri na mpiga ngoma wao toka Mbeya,sijawahi kuona mikoa mingine ikiiga hata nusu ya hawa jamaa nadhani mpira utaendelea sana hapa Tanzania”alisema Shija.


katika mchezo huo Mbeya City walishinda 1-0 na baada ya mchezo kumalizika mashabiki hao waliingia katikat ya uwanja na kucheza na kuimba kwa muda mrefu sana kwa furaha.Akiongea baada ya mchezo huo kocha wa timu hiyo alisema "namshukuru Mungu kwa kuweza kutusaidia kushinda mchezo huu,pia nawashukuru sana wachezaji wangu kwa kucheza kama nilivyowaelekeza,na kikubwa kilichotusaidia ni nidhamu kubwa iliyoonyeshwa na wachezaji ndani ya uwanja kwani kwa hali ya kawaida presha waliyokuja nayo JKT baada ya kufungwa ilikua kubwa sana wahezaji wasingetuliza vichwa hali ingekua nyingine,hivyo wachezaji wamefanya kazi kama walivyoelekezwa,pia napenda sana kuwashukuru watu wa Mbeya kwa sapoti wanayozidi kutupa kwani inatupa faraja sana na kujiona tuna deni la kulipa,tunawashukuru sana na tutajitahidi tusiwaangushe"
                                      OYOOOOOOOOO
Nae shabiki aliyesafiri kuifata timu toka Mbeya aliyejitambulisha kwa jina la Maka alisema "kwa muda mrefu Mbeya tunajiamini tuna wachezaji wengi wazuri,na vle vile tunajiamini tunapenda sana  mpira,sasa hivi watu wamegundua,unajua miaka ya zamani wakati timu za Tukuyu Stars na Mecco zilipokua juu watu wengi walikua wanahisi zina mapenzi na timu za Yanga na Simba hivyomara nyingi mtu ulikua unajua kuwa mechi hii watafungwa na mechi hii matokeo yanaweza kua tofauti,lakini sasa hivi hawa Mbeya City wanatupa raha sana maana wanakomaa kila mech,hakuna cha Siba wala Yanga,zibaki huko huko na mipira yao ya mdomoni...maana wanavyosifiwa katika magazeti ni tofauti na uhalisia...sisi ndio Mbeya hatutaki sifa ni kazi kwenda mbele"alimalizia huku akiwafata wenzake na kuendelea kucheza.
TUMESHINDA.....

Sunday, 6 October 2013

Tz Prison yaifunga Mgambo shooting 1-0

                                                             Tz prison
Timu ya TZ PRISON imefanikiwa kupata ushindi muhimu wa ugenini dhidi  ya timu ya Mgambo Shooting  ya Tanga katika mchezo mzuri uliochezwa katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.Katika mchezo huo Tz Prison  ilitawala sana kipindi cha kwanza na kufanikiwa kulisakama  mno goli la Mgambo,lakini uhodari wa mabeki uliwasaidia kutokufungwa mapema.hadi kipindi cha kwanza kinakwisha  hakuna timu iliyo fanikiwa kupata bao.

Tz Prison walikianza kipindi cha pili kwa nguvu zaidi na kufanikiwa  kupata goli katika dakika ya 65 baada ya kazi nzuri ya Julius Hamisi aliyekimbia na mpira na kupiga krosi nzuri iliyomkuta  Peter Michael aliyeukwamisha wavuni.Tz Prison waliendelea kulisakama goli la Mgambo na kukosa nafasi kadhaa.hadi mchezo unakwisha  Tz Prison  waliondoka na ushindi wa goli moja kwa bila.
TZ PRISON KUWAVAA MGAMBO JKT LEO
                 IMEANDIKWA NA ABDUL SUDI

                                                                                KIKOSI CHA TANZANIA  PRISON
Timu ya Tz Prison ya Mbeya leo inacheza na timu ya Mgambo JKT katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.mchezo huo utafanyika katika uwanja wa mkwakwani Tanga.Tanzania Prison inashika nafasi ya 13 ikiwa na point 4 baada ya kufungwa michezo miwili na ruvu shooting na ruvu jkt,kabla ya kutoka sare michezo minne na timu za  coastal union 0-0,Yanga 1-1,Mtibwa 1-1,na pia kutoka sare na Azam kwa goli 1-1,wakati timu ya Mgambo inashika nafasi ya 12 ikiwa na point 5 baada ya kupoteza mechi mbili walipofungwa na Ruvu Shooting 1-0,kisha wakaja kuaibishwa na  Simba 6-0,wakatoa sare na oljoro 0-0,na Rhino 1-1 na kushinda mechi moja dhidi ya Ashant kwa kuifunga goli 1-0.
Mchezo huo ni muhimu sana kwa Tz Prison kwani inahitajika lazima ishinde ili ijiweke katika mazingira mazuri na kuongeza imani kwa mashabiki wake walioanza kurudi kwa kasi kuisapoti timu hiyo.Kwa mujibu wa viongozi waliofatana na timu,wachezaji wapo   katika hali nzuri na jana walifanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa mkwakwani.Wachezaji wote wana ari na mchezo huo na wamepania kucheza kwa juhudi zote ili wazipate point zote tatu.
Kikosi cha Tz Prison kitakachoanza leo ni
1.BenoDavid
2.Salum Kimenya
3.Boniface Hau
4.Jumanne Elfadhili
5.Nurdin Issa
6.Jimmy Shoji (GEMMA)
7.Jeremiah Juma
8.Omega Seme
9.Peter Michael
10.Ibrahim Isaka
11.Julius Khamis.
Wachezaji wa akiba ni Albert Mweta,Laurian Mpalile,Lugano Mwangama,Fredy Chudu,John Matei,Six Mwasekaga.
KILA LA HERI TANZANIA PRISON