Friday, 1 November 2013

Yanga yanoga

       Timu ya Yanga imeweza kuwafunga Ruvu JKT kwa magoli 4-0 katika mchezo wa upande mmoja ambapo Yanga waliutawala mchezo huo katika vipindi vyote viwili.
     Yanga walipata goli la kwanza mapema katika kipindi cha kwanza  lililofungwa na Mrisho Ngasa baada ya kupata pasi toka kwa Domayo  na akawahadaa mabeki wa Yanga  wakidhani anataka kutoa pasi  ndipo alipopiga shuti kali lililomshinda kipa wa JKT  na kuingia golini.
      JKT hawakuonyesha kutulia na mabeki wake walikua kila mara wakijichanganya na kuwafanya Yanga wazidi kutawala mchezo, goli la pili lilifungwa tena na Mrisho Ngasa baada ya mpira uliorushwa na Mbuyu Twite kuwapita mabeki wa JKT na ukadunda na kumkuta Ngasa aliyepiga kichwa na kuandika goli la pili.
      JKT walicheza bila ya maelewano na hasa viungo wao waliokua wakipoteza mipira mara kwa mara na kuwafanya viungo wa Yanga kua na kazi rahisi ya kusambaza mipira kila upande.
   Yanga walipata goli la tatu kupitia kwa beki wake wa kushoto Oscar Joshua baada ya kona iliyopigwa na Ngasa kuokolewa kizembe na mabeki wa JKT na mpira kumkuta Joshua aliyepiga shuti zuri la mguu wa kushoto na kuandika goli la tatu

      Waliendelea kushambulia na mshambuliaji wake Jerry Tegete alikosa nafasi tatu za wazi kufunga magoli na baadae kufanikiwa kufunga baada ya kuukuta mpira uliowapita mabeki wa JKT na kuandika goli la nne.hadi mpira unamalizika Yanga wakaondoka na ushindi wa magoli manne kwa bila. 

Tuesday, 29 October 2013

     mbeya city yashinda
   Mbeya derby
                                                 NA ABDUL SUDI,MBEYA

               Timu ya Mbeya City imefanikiwa kutoka na ushindi mnono wa magoli 2-0 dhidi ya wapinzani wao wakubwa timu ya  Tz Prisons  ya hapo hapo jijini Mbeya,  katika mchezo mkali uliojaa kila aina ya ufundi.
              Katika mchezo huo,  muamuzi Israel Mkongo toka Dar es salaam alimudu vilivyo na kusifiwa na mashabiki waliotazama mchezo huo.
ISRAEL MKONGO

                 Hadi timu hizo zinakwenda mapumziko zilikua bado hazijafungana ingawa kosa kosa zilikua nyingi kwa kila timu.
KOCHA WA MBEYA CITY JUMA MWAMBUSI
       Prison ndio walioanza kutawala dakika za mwanzo kwani walifanya mashmbulizi mengi ingawa safu ya ulinzi ya Mbeya City iliyokua ikiongozwa na  Yusuph Abdallah na Deoratius Julius walifanya kazi nzuri ya kuwazuia washambuliaji wa Prison na hasa  Peter Michael aliyekua akiwasumbua mara kwa mara.
MBEYA CITY
                    Nao Mbeya City walizinduka na Alex Seth alifanya kazi nzuri mara kadhaa ya kuwatoka mabeki wa Tz Prisons na kupiga krosiambazo zilikkua zikiokolewa.
            Kipindi cha pili Prison walianza tena kwa kasi na kukosa goli la kuongoza baada ya kufanya shambulizi kali na mpira uliookolewa na mabeki wa Prison ulimkuta Peter Mapunda aliyepiga shuti kali na kuandika goli la kwanza.
TZ PRISONS
                 Mbeya City waliendelea kushambulia na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa kwa njia ya penati baada ya beki wa Prison kumfanyia madhambi shambuliaji wa Mbeya City Deus Kaseke,na Deogratus Julius akafunga penati hiyo.
WACHEZAJI WA MBEYA CITY WAKISHANGILIA GOLI LA KWANZA

                  Kwa kiasi kikubwa mabadiliko yaliyofanywa na kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi ya kumbadilisha Jeremiah John aliyeumia na nafasi yake kuchukuliwa na Mwagane Yeya,na kkumtoa chipukizi Alex Seth na nafasi yake kuingia Peter Mapunda ndio yaliyobadilisha kabisa hali ya mchezo huo, kwani mashambulizi yaliongezeka na kufanikiwa kupata mabao yote mawili.

Monday, 28 October 2013

Azam yaitoa nishai simba

           Azam imeweza kutumia udhaifu wa timu ya Simba na kuweza kuwashinda kwa magoli 2-1,  katika  mchezo mzuri wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa katika uwanja wa taifa Dar es salaam.
              Hadi kipindi cha kwanza kinakwisha timu hizo zilikua zmefungana goli moja kwa moja.Simba ilikua ya kwanza kupata bao lililofungwa na Ramadhani Singano baada ya kazi nzuri iliyofanywa na kiungo wa kati wa Simba Said Ndemla kupiga pasi ya pembeni iliyomkuta  Zahor Pazi aliyempita kirahisi beki wa kushoto wa Azam Wazir Seif na kupiga krosi  ndogo iliyomkuta  Singano aliyewahamisha mabeki wa Azam na kupiga shuti lililopita kushoto mwa goli la Simba na kuandika goli la kwanza.
ZAHORO PAZI AKIKIMBIA KUSHANGILIA BAADA YA KUTOA PASI YA GOLI LA KWANZA LA SIMBA
      Azam hawakutetereka na goli hilo kwani walifanya shambulizi kubwa na pasi ndefu ya Abubakar Salum ilimkuta John Boko aliyemzidi nguvu beki wa Simba Hassan Hatibu na kupiga shuti lililotoka nje.
          Simba ilikua ikifanya mashambulizi mengi kupitia kwa Singano ambae mara kwa mara alikua akimsumbua Said Morad na dakika ya 34  alipiga pasi  nzuri iliyomkuta Zahor Pazi aliyeingia nao katika eneo la hatari na alippotaka kupiga aliwahiwa na Agrey Moris na kua kona ambayo haikuzaa matunda.
WACHEZAJI WA SIMBA WAKISHINGILIA GOLI LAO

           Azam walisawazisha kutokana na mpira uliotoka katikati ya uwanja  na Kipre Balou alipiga pasi upande wa kulia mwa uwanja ukamkuta Abubakar aiyempigia pasi  Erasto Nyoni ambae alimaliza uwanja na kupiga pasi nzuri iliyomkta Kipre Tcheche aliyeukwamisha wavuni.
            Kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko  kwa kumtoa Zahor Pazi na Amri Kiemba na nafasi zao kuchukuliwa na Christopher Edward na Sino Augustino wakati Azam walimtoa Said Morad na Josef Kimwaga na kuwaingiza David Mwantika na Malick mabadiliko yaliyowasaidia sana Azam, kwani Mwantika aliweza kumzuia Singano vizuri na kuziba njia zote za kupenyeza mipira.
RAMADHANI SINGANO AKIJIPANGA KUMTOKA SAID MORAD
        Azam walipata bao la pili kupitia tena kwa Kipre Tcheche  aliyepigiwa pasi ndefu na Abubakar Salum na kumpita kirahisi Wiliam Lucien na kuupiga mpira kiufundi na kupita pembeni mwa lango la Simba na kuandika bao la pili.
       Simba walipata nafasi ya kuswazisha goli hilo baada ya Mombeki kumpigia pasi nzuri Sino lakini akashindwa kufunga.
SINO AUGUSTINO,SURE BOY,MWANTIKA NA PEMBENI BALOU WAKIMPITA CHISTOFER EDWARD ALIYEUMIA
 Kwa ujumla  Simba hawakucheza vizuri kabsa katika mchezo wa huo  kwani mabeki wake wa kati  Owino na Hassan Hatibu walikua hawaelewani mara kwa mara na hata Wiliam Lucien aliyecheza kama beki wa kulia alisumbuliwa sana na Kipre Tcheche, hadi sasa timu ya Simba bado haijapata kikosi cha kwanza  na hilo linawasumbua sana.     
KOCHA WA AZAM AKIONGEA NA CAPTAI WA SIMBA KATIKA MECHI HIYO, OWINO
            

                     Na hata mabadiliko waliyofanya hayakuwasaidia sana lakini Azam walifanya mabadiliko na yalisaidia kuongeza nguvu na ufundi hadi wakafanikiwa kupata ushindi.

Sunday, 27 October 2013

Torres awamaliza man city

        Fernando Torres ameweza kusaidia kutoa pasi ya goli la kwanza na kufunga la pili na kuiwezesha timu yake ya Chelsea kuifunga Man City kwa magoli 2-1.

        Katika mchezo huo ambao ulikua mgumu na kila mmoja akitarajia kuwa utaisha kwa sare ya goli 1-1 Torres alitumia vizuri makosa yaliyofanywa na beki wa City Matija Natascic na kipa wake Joe Hart kuchanganyana  na mpira kumkuta Torres aliyefunga kirahisi.
             Aguero aliisawazishia  City baada ya kupata pasi nzuri toka kwa  Samir Nasri na akapiga mpira uliokwenda pembeni mwa goli na kuandika goli.

   Goli hilo liliwafanya Man City kuendelea kushambulia na Aguero alikosa tena goli la wazi pale mabeki wa Chelsea walipodhani ameotea lakini alipojaribu kuubetua mpira ukatoka nje. Na shuti kali la Ramirez aliyekua akihaha uwanja mzima lilitoka nje idogo ya goli la City.


     Gary Cayhil nusura aipatie timu yake goli lakini alipobaki na kipa wa City Joe Hart,  aliupaisha mpira kwa mshangao wa wengi.

                       Torres aliyecheza vizuri sana katika mchezo huo aliweza kuipa ushindi timu yake alipofunga dakika ya tisini ya mcezo na kuifanya itoke uwanjani kwa ushind wa 2-1.

                Kocha wa Chelsea alishindwa kujizuia kwa furaha na kukimbia had kwa masahbiki wa timu hiyo na kushangilia pamoja nao..