Tuesday, 8 October 2013

ADNAN JANUZAJ
KINDA LA MAN UTD

Adnan Januzaj  amecheza mechi moja tu kamili toka ajiunge na timu ya Manchester United,lakini nchi tano zote zinataka akachezee timu zao za taifa.Nchi za Uturuki,Serbia,Kosovo na Albania pamoja na nchi aliyozaliwa ya Ubelgiji zote zinataka azichezee,na hata Uingereza nao wameanza  kampeni za chini chini za kutaka kumchukua ili awe raia wa nchi yao.
Januzaj alizaliwa Ubelgiji,ingawa wazazi wake walitokea Albania,ingawa nao kwao ni Kosovo.na walikuwa wamekimbia vita hivyo wakapata uraia wa Ubelgiji.
Alichukuliwa na timu ya Anderlecht ya ubelgiji alipokua na miaka 10 na akakaa hapo hadi alipofikisha miaka 16 ndipo akachukuliwa na Manchester United.Wakati kocha wa zamani wa Manchester United anataka kujiuzulu alimkabidhi Januza jezi namba 44.Mechi yake ya kwanza ilikua ni katika kombe la ngao ya hisani dhidi ya Wigan alipoingia badala ya Van Persie,nay a pili alimbadili Ashley Young walipocheza na  Crystal Palace,na mechi ya tatu ambayo alianza toka mwanzo ni walipocheza na Sunderland na akafanikiwa kufunga magoli yote mawili waliposhinda 2-1.

Ni mchezaji mwenye kasi,anaetumia sana mguu wa kushoto,anapiga chenga na anajua kufunga.alifanya vizuri sana wakati wa michezo ya majaribio kabla ya kuanza kwa msimu huu,na ingawa bado ana umri mdogo wa miaka 18 tayari kishaonyesha atakua ni mmoja kati ya wachezaji wazuri sana duniani.
 Ingawa nchi zote hizo zinataka akachezee timu zao za taifa lakini mwenyewe bado hajaamua akacheze wapi,lakini baba yake anasema atafurahia sana kama akiichezea nchi ya Albania.

No comments:

Post a Comment