Wednesday, 9 October 2013

MBEYA CITY KUCHEZA NA RHINO

                                                                                                MBEYA CITY FC
Timu ya Mbeya City leo inacheza na timu ya Rhino ya Tabora katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara,mchezo huo unatarajiwa kuchezwa katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.Akiongea na Mbeya Maskan kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi amesema timu katika hali nzuri,na wanatarajia mchezo utakua mgumu na mzuri kwani wanaiheshimu Rhino kwa jinsi wanavyocheza lakini wamejitayarisha vizuri kukabiliana nao,na mungu akipenda atashnda.Hadi sasa Mbeya City imecheza mechi tatu ugenini,dhidi ya Mtibwa wakatoka sare ya 0-0,kisha wakacheza na Simba pia wakatoa sare ya 2-2 kabla hawajacheza na Oljoro na kuifunga 1-0.Mbeya City wamepania kushambulia sana katika mchezo wa leo,kwani wanahitaji point tatu ili wazidi kusogea juu zaidi katika msmamo wa ligi kuu.Mbeya City wanashika nafasi ya 11 wakiwa na point 11,wakishinda leo watapishana kwa pointi moja na kinara wa ligi hiyo Simba wenye pointi 15.
KIKOSI CHA MBEYA CITY LEO KITAKUA
1.David Baruan
2.John Kabanda
3.Hassan Mwasapile
4.Deo Julius
5.Anthony Mayunga
6.Yusuph Abdallah
7.Alex Setth
8.Steven Mazanda
9.Paul Nonga
10.Jeremiah John
11Deus Kaseke.

KILA LA KHERI MBEYA CITY.

No comments:

Post a Comment