tatizo nini
MAN UNITED?
imeandikwa na Abdul(be good) Sudi,Mbeya
Kabla hajajiuzulu,aliyekua kocha wa Manchester united,sir Alex Ferguson alisema ameiacha timu ikiwa katia kiwango cha juu sana,lakini toka aje David Moyes kikosi kimebaki kile kile,lakini had sasa baada ya michezo sita imeejikuta iko katika nafasi ya 12,nafasi ya chini kuwahi kufika kwa muda mrefu sana.toka mwaka 1989.
Kabla hajajiuzulu,aliyekua kocha wa Manchester united,sir Alex Ferguson alisema ameiacha timu ikiwa katia kiwango cha juu sana,lakini toka aje David Moyes kikosi kimebaki kile kile,lakini had sasa baada ya michezo sita imeejikuta iko katika nafasi ya 12,nafasi ya chini kuwahi kufika kwa muda mrefu sana.toka mwaka 1989.
Tatizo ni nini??hiki ndio kikosi kilichochukua ubingwa
ligi kuu msimu uliopita,je tatizo n wachezaji wamechoka au tatizo liko kwa
kocha David Moyes??
Ukitazama sana toka msimu uliopita timu ilionyesha
kwamba inahitaji viungo,lakini hadi dakika za mwisho wakati dirisha la usajili
linataka kufungwa ndio akasajiiwa Marouane Fellaini,hivyo hajapata muda wa kukaa sana na wenzake
kabla ligi hajaanza kucheza,hvyo bado anahitaji muda wa kuchanganya.
Wachezaji wakongwe
kama Ryan Gigs,Rio Ferdinand,Nemanja Vidic na hata Carrick wanashidwa kwenda na
kasi ya mchezo hivyo inawapa shida sana pale wanapokutana na timu zinazojua
kufanya mashambulizi ya kushtukiza “counter attack,
Kuna tatizo la majeruhi wanaotokea mara kwa mara,kama
ilivyotokea kwa Rafael da Silva na kuwafanya wachezaji kama Phil Jones na Chris
Smalling kupangwa pembeni hivyo kwa vile hawana mazoea ya kucheza nafasi hiyo
timu inashindwa kushambulia na silaha kubwa sana kwa man ni kushambulia toka
pembeni.
Na kikubwa kinachowasumbua mashabiki ni kwa nini hamchezeshi Shinji Kagawa kama kiungo wa juu,kwani alipokua Borusia Dotmund alikua akiicheza nafasi hiyo na kufunga magoli mengi mno na kutoa pasi nyingi za magoli,lakini hakuna anaeelewa kwa nini Moyes hamuamini,na hata akimpanga anamuweka nafasi ambayo si yake,pembeni kitu kinachofanya ashindwe kucheza vizuri.inashangaza kuona timu inasumbuliwa katika kiungo wakati katika benchi kuna kiungo wa kiwango cha juu.
Na kikubwa kinachowasumbua mashabiki ni kwa nini hamchezeshi Shinji Kagawa kama kiungo wa juu,kwani alipokua Borusia Dotmund alikua akiicheza nafasi hiyo na kufunga magoli mengi mno na kutoa pasi nyingi za magoli,lakini hakuna anaeelewa kwa nini Moyes hamuamini,na hata akimpanga anamuweka nafasi ambayo si yake,pembeni kitu kinachofanya ashindwe kucheza vizuri.inashangaza kuona timu inasumbuliwa katika kiungo wakati katika benchi kuna kiungo wa kiwango cha juu.
UPANDE wa pembeni Luis Nani peke yake ndio anacheza
kwa kiwango cha juu,lakini Ashley Young bado hajaonyesha kama ana sifa ya kua
ni mchezaji wa timu kubwa kama ya Manchester United,na hata Valencia sio Yule wa misimu miwili iliyopita
bado hajaonyesha makali yake hivyo timu inashindwa kupata mipira ya kutokea
pembeni kama ilivyokua misimu iliyopita,angalau upande wa Evra ndio anaweza
kuleta pasi kadhaa za magoli.
Ukitazama kwa makini ,kocha ana sababu nyingi sana za
kulaumiwa kwani alipochukua nafasi,ilitakiwa abaki kwanza na wasaidizi wa
Ferguson katika benchi la ufundi ili
wamuonyeshe njia lakini akaamua kuleta watu wapya ambao hadi sasa inaonekana
wanashindwa kumshauri vizuri,ndio maana timu inasumbuka na anashindwa hata
kuibadili,ikumbukwe wakati wa ferguson alikua akiweza kuubadili mchezo katika
dakika 15 za mwisho,na hakuna siku hata moja Manchester iliwahi kuelemewa
mwanzo hadi mwisho, ukiondoa walipocheza na Barcelona,lakini sasa hivi kila
ikicheza mashabiki wake wanakua na wasiwasi,maana wanakua hawana uhakika wa
ushindi.





No comments:
Post a Comment