Saturday, 5 October 2013

MBEYA CITY KUWAVAA OLJORO JKT


                NA ABDUL SUDI.
Ligi kuu ya Vodacom Tanzania inaendelea jumamosi hii  kwa timu ya Mbeya City,kucheza na timu ya JKT Oljoro  katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Arusha katika mchezo unaotarajiwa kuwa mkali na wa kuvutia.Timu ya JKT Oljoro ipo katika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi baada ya kushinda mechi moja na kutoa sare michezo miwili na kupoteza mitatu,wakati timu ya Mbeya City inashika nafasi ya nane ikiwa na point 8 baada ya kushinda mchezo mmoja na kutoka sare michezo mitano.
Kocha wa timu ya Mbeya City Juma Mwambusi  amesema kikosi kipo katka hali nzuri na anategemea ushindi katika mchezo wa leo,anasema hana wasiwasi na majeruhi kwani timu yake inacheza kitimu zaidi ya kumtegemea mtu mmoja mmoja “wachezaji wa Mbeya City wote wapo katika kiwango sawa,kwa vile wanacheza kitimu,hatumtegemei mchezaji mmoja mmoja ndio maana utaona hata nikifanya mabadiliko anaeingia anakua na uwezo ule ule kama wa yule aliyetoka,hivyo inakua rahisi kuunganisha na wenzake”.alisema alisema kocha  Mwambusi.
                      KILA LA HERI MBEYA CITY
       

No comments:

Post a Comment