Tz Prison yaifunga Mgambo shooting 1-0
Tz prison
Timu ya TZ PRISON imefanikiwa
kupata ushindi muhimu wa ugenini dhidi
ya timu ya Mgambo Shooting ya
Tanga katika mchezo mzuri uliochezwa katika uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.Katika
mchezo huo Tz Prison ilitawala sana
kipindi cha kwanza na kufanikiwa kulisakama mno goli la Mgambo,lakini uhodari wa mabeki
uliwasaidia kutokufungwa mapema.hadi kipindi cha kwanza kinakwisha hakuna timu iliyo fanikiwa kupata bao.
Tz Prison walikianza kipindi
cha pili kwa nguvu zaidi na kufanikiwa
kupata goli katika dakika ya 65 baada ya kazi nzuri ya Julius Hamisi
aliyekimbia na mpira na kupiga krosi nzuri iliyomkuta Peter Michael aliyeukwamisha wavuni.Tz Prison
waliendelea kulisakama goli la Mgambo na kukosa nafasi kadhaa.hadi mchezo
unakwisha Tz Prison waliondoka na ushindi wa goli moja kwa bila.

No comments:
Post a Comment