Sunday, 6 October 2013

TZ PRISON KUWAVAA MGAMBO JKT LEO
                 IMEANDIKWA NA ABDUL SUDI

                                                                                KIKOSI CHA TANZANIA  PRISON
Timu ya Tz Prison ya Mbeya leo inacheza na timu ya Mgambo JKT katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara.mchezo huo utafanyika katika uwanja wa mkwakwani Tanga.Tanzania Prison inashika nafasi ya 13 ikiwa na point 4 baada ya kufungwa michezo miwili na ruvu shooting na ruvu jkt,kabla ya kutoka sare michezo minne na timu za  coastal union 0-0,Yanga 1-1,Mtibwa 1-1,na pia kutoka sare na Azam kwa goli 1-1,wakati timu ya Mgambo inashika nafasi ya 12 ikiwa na point 5 baada ya kupoteza mechi mbili walipofungwa na Ruvu Shooting 1-0,kisha wakaja kuaibishwa na  Simba 6-0,wakatoa sare na oljoro 0-0,na Rhino 1-1 na kushinda mechi moja dhidi ya Ashant kwa kuifunga goli 1-0.
Mchezo huo ni muhimu sana kwa Tz Prison kwani inahitajika lazima ishinde ili ijiweke katika mazingira mazuri na kuongeza imani kwa mashabiki wake walioanza kurudi kwa kasi kuisapoti timu hiyo.Kwa mujibu wa viongozi waliofatana na timu,wachezaji wapo   katika hali nzuri na jana walifanya mazoezi ya mwisho katika uwanja wa mkwakwani.Wachezaji wote wana ari na mchezo huo na wamepania kucheza kwa juhudi zote ili wazipate point zote tatu.
Kikosi cha Tz Prison kitakachoanza leo ni
1.BenoDavid
2.Salum Kimenya
3.Boniface Hau
4.Jumanne Elfadhili
5.Nurdin Issa
6.Jimmy Shoji (GEMMA)
7.Jeremiah Juma
8.Omega Seme
9.Peter Michael
10.Ibrahim Isaka
11.Julius Khamis.
Wachezaji wa akiba ni Albert Mweta,Laurian Mpalile,Lugano Mwangama,Fredy Chudu,John Matei,Six Mwasekaga.
KILA LA HERI TANZANIA PRISON

No comments:

Post a Comment