Friday, 28 February 2014

YANGA VITANI NA AL AHLY

Yanga ya Tanzania, jumamosi inakutana na mabingwa wa Misri Al Ahly katika mchezo wa kwanza wa klabu bingwa Africa, Mchezo huo utachezwa katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.

    Katika mchezo huo, Yanga wanatakiwa kushinda kwa idadi yoyote ya magoli kwani  si rahisi kuzifunga katika viwanja vyao, hivyo inatakiwa Yanga wahakikishe wanapata ushindi mnono hapa hapa nyumbani.
    Kikosi cha Yanga kina wachezaji wengi wenye uzoefu wa michezo mikubwa, kama Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Mrisho Ngasa, Didier Kavumbagu, Athman Iddi, Hamis Kiiza, na sasa hivi ameongezeka Emanuel Okwi, hivyo haina haja ya kuogopa timu pinzani.
EMANUEL OKWI
       Yanga wana washambuliaji wakali sana lakini ina mapungufu katika ulinzi ambayo nina uhakika hadi sasa kocha tayari atakua ameyafanyia kazi, tatizo dogo lililopo kwa timu hiyo ni kwamba hawana beki wazuri wa pembeni kwani Oscar Joshua na Mbuyu Twite katika siku za karibuni hawako katika viwango vizuri, lakini kama wakituliza akili wana uwezo mkubwa sana wa kuwazuia  Ahly.
        Timu ya Al Ahly inategemewa kucheza mchezo wa jumamosi kama wanavyocheza katika michezo mingi wakiwa ugenini, wanaulinda sana mpira na kupiga pasi nyingi sana  ili kuwapoza na kuwafanya mjisahau kisha hua wanashambulia kwa haraka sana na mara nyingi anaeanzisha mashambulizi anakua ni beki wa pembeni, hivyo Yanga wawe makini sana na aina hiyo ya uchezaji.
AL AHLY WAKIWA MAZOEZINI IST
   Lakini kwa Yanga timu yao ina washambuliaji wote wenye kasi sana, nan i rahisi wakipata nafasi kuzitumia. Mchezaji kama Simon Msuva kwa sasa hivi yuko katika kiwango cha juu sana hivyo anatarajiwa kuwapelekea mipra mara kwa mara kina Okwi na Kavumbagu ili wapachike magoli.

     Mungu ibariki Yanga ishinde.

No comments:

Post a Comment