Saturday, 1 March 2014

yanga
yawaduwaza al alhly

      Klabu bingwa ya Tanzania Yanga, leo imevunja mwiko baada ya kuwafunga Al Ahly yaa Misri goli moja kwa bila katika mchezo wa klabu bingwa Afrika. Toka waanze kukutana mwaka 1982, hii ni mara ya kwanza kwa Yanga kushinda.

         Nahodha wa Yanga Nadir Haroub aliipatia timu yake goli hilo muhimu dakika nane kabla mchezo huo haujamalizika.
     Katika mchezo huo Yanga waliutawala kwa kipindi kirefu ambapo Mrisho Ngasa, Emanuel Okwi, Simon Msuva na Hamisi Kiiza walikua wakiwasumbua muda mrefu walinzi wa Al Ahly.
MASHBIKI WA YANGA WAKIWA WAMEKAA UPANDE WA SIMBA 
       Simon Msuva  alikaribia kufunga katika dakika ya 18 lakini mpira aliopiga uliokolewa kiufundi na kipa wa Ahly,  dakika moja baadae Emanuel Okwi nae alipiga kichwa kilichookolewa na kipa  
     Dakika ya 26 Hamisi Kiiza alikosa bao la wazi baada ya kazi nzuri iliyofanywa na Msuva lakini akaupiga mpira uliotoka nje.

   Ingawa hatari hazikua nyingi upande wa Yanga, lakini walinzi wake walicheza vizuri sana katika mchezo huo hasa nahodha wao  Haroub alieza kuwainda vema washambuliaji wa Ahly wasilete madhara.
      Goli la Yanga lilipatikana baada ya juhudi za mshambuliaji wake Emanuel Okwi aliyeingia na mpira katika eneo la hatari ndipo walinzi wa Ahly waautoa ikawa kona, na Msuva akapiga kona nzuri iliyomkuta Nadir Harou aliyepiga kichwa kifundi na mpira ukamshinakipa wa Al Ahly Sherif Ekramy na kuingia golini.

    Al Ahly waliwachezesha washambuliaji wawili, Mohamed Nagy "Gedo"na Amr Gamal huku  wakimuanzisha kiungo wake mpya toka Burkina Faso Musa Yedan lakini hawakua na mipango mizuri ya kuipenya ngome ya Yanga iliyoongozwa na Nadir Haroub ambae alicheza vizuri sana katika mchezo huo.


 Katika mchezo huo Yanga walionyesha kiwango cha hali ya juu na walikua wakifanya mashambulizi yenye mpngilio lakini uimara wa walinzi wa Ahly uliwafanya washindwe kupenya na kufunga magoli mengi.
     Mchezo wa marudiano  utafanyika jumapili ijayo jijini Cairo.

No comments:

Post a Comment