Sunday, 23 March 2014

Kutoka mbeya hadi chamazi…….

Mamia ya mashabiki wa Mbeya City, walisafiri  toka jijini Mbeya kuifuata timu yao ilipokua ikicheza na JKT Ruvu(ruvu stars)katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi jijini Dar.
    Kama ilivyokua kwa michezo mingi,  timu yao haikuwaangusha mashabiki wake, kwani ilishinda kwa magoli mawili kwa bila, magoli yote yakipachikwa na mmoja kati ya washambuliaji wake hatari Saad Kipanga.

      Magoli hayo aliyafunga moja kila kipindi,  lakini yote mawili kwa mashuti. La kwanza alilifunga dakika ya tisa baada ya kukutana na mpira wa Mwegane Yeya uliookolewa na mabeki baada ya shambulizi kali na kumkuta mfungaji aliyepiga fataki kali llilomshinda kipa mzoefu wa JKT Shaaban Dihile.
      La pili lilikua zuri zaidi, kwani baada ya JKT kushambulia  kwa nguvu ili kutafuta bao la kusawazisha, walijisahau nyuma na mpira mrefu uliopigwa  na mabeki wa City ulimkuta Paul Nonga aliyekua peke yake na mabeki wa JKT, aliutuliza mpira na kuwasubiri wenzake kisha akampasia Mwegane nae akamuwekea Kipanga aliyepiga shuti kali zaidi la mguu wa kushoto na  kutinga moja kwa moja wavuni na kuandika bao la pili.
    City waliutawala sana mchezo hasa kipindi cha kwanza na walifanya mashambulizi mengi langoni mwa JKT, na kama wangeku makini zaidi wangeweza kupata ushindi mkubwa zaidi.

       Pamoja na ushindi huo, lakini burudani ilikua ni kwa mashabiki wake waliokua wakishangilia kuanzia mwanzo hadi mwisho wa mchezo huo bila kuchoka.

     ‘Tunaona fahari sana kuishangilia timu yetu, inatupa furaha na umoja ambao ni vigumu sana kuutenganisha” aliongea shabiki mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Joe Mwakatumbula aliyetokea  kwa mama John jijini Mbeya. “nimesafiri kutazama michezo yote ya Mbeya City, ni mmoja tu niliukosa siku walipocheza na Rhino Tabora, na ilikua ni kwa sababu nilipata msiba, lakini sijakosa mchezo mwingine wowote wa Mbeya City” aliongeza kwa furaha.


       Nae   John Mwakalebela ambae ametokea maeneo ya Airport alisema “hii ni timu yetu watu wa Mbeya hatuna budi kuipa sapoti kila tunavyoweza maana inawakilisha vizuri  jiji letu, na kikubwa kinachofurahisha, wanajituma kwa juhudi sana na kutupa raha tunyoitarajia”alimalizia Mwakalebela.
   Pia kulikua na kina dada kadhaa ambapo mmoja wao aliyejitambulisha kwa jina la Lucy Kalinga alisema " nimesafiri toka Mbeya hadi Dar, lakini nimeridhika na kiwango cha timu na matokeo tuliyopata,  kwa sasa nguvu yetu tunaipeleka katika mchezo unaofuata dhidi ya wapinzani wetu wa jadi Tz Prisons, na tuna uhakika wa ushindi, lazima tupate nafasi mbili za juu"alitamba dada Lucy.

No comments:

Post a Comment