MECHI YA
KARNE
Tz Prisons
na Mbeya city
IMEANDIKWA
NA JOEMAN JOH, MBEYA/picha toka vyanzo mbali mbali.
Jumapili
tarehe 30,Machi,2014 kutakuwa na mchezo
wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania kati ya Tz Prisons dhidi ya Mbeya City. Hiyo ni
Mbeya derby kwani wote ni watoto wa jijini Mbeya na hata mitaa zinapotoka timu
hizi siyo mbali.
Mchezo huu unazikutanisha timu mbili
zikiwa na malengo tofauti, City inataka kuzikimbilia YANGA na AZAM kwenye
kilele cha ligi, wakati Tanzania Prisons inakimbia kusalimisha roho yake, kwani
ipo katika hatari ya kushuka daraja.
![]() |
| TZ PRISONS |
Wakati
City wakiwa nafasi ya tatu katika msimamo waligi, Prisons hadi sasa iko nafasi
ya 10 kati ya timu 14. Lakini ukiondoa kipigo cha kushtukiza walichokipata toka
kwa Yanga, wapo vizuri sana ki uchezaji na ari ya kimchezo.
Toka mzunguuko wa pili uanze Prisons
wamepoteza michezo miwili tu, kwa Kagera na Yanga, na zote wamepoteza ugenini,
lakini zilizobaki wamefanya vizuri.
Upande
wa pili City imeshinda
mechi zake zote mbili za mwisho dhidi ya RHINO (Sokoine) na dhidi ya JKT
Ruvu(Chamazi).Kutokana na matokeo hayo na yale ya mechi ya kwanza baina yao
ambapo City walishinda 2-0 yanaleta taswira ya jinsi gani mechi hii itakavyokuwa
ngumu...
![]() |
| MBEYA CITY |
Kingine kinacholeta ugumu wa mechi ni
malengo yao pamoja ufundi wa makocha Juma Mwambusi na David Mwamwaja ambaye
kaibadilisha Prison kuwa timu inayocheza vizuri tofauti na awamu ya kwanza..
City wanaoongozwa na kocha Juma Mwambusi, wanacheza mpira wa kasi na wanatumia
sana walinzi na viungo wao wa pembeni, John Kabanda,Hassan Mwasapili, Deus
kaseke na Peter Mapunda kuanzisha mashambulizi, pia wana wafungaji wengi wazuri
kwani hadi sasa tayari kuna washambuliaji wanne wamepokezana kufunga magoli,
Mwegane Yeya, Peter Mapunda,Richard Peter(ambae ni majeruhi) na Saad Kipanga, pia Paul Nonga ni
mpiganaji mzuri sana na ni tatizo kwa kila beki anaekutana nae. washambuliaji
hao ni wazuri sana kwa kucheza mipira ya juu.
![]() |
| KOCHA WA MBEYA CITY, JUMA MWAMBUSI |
Tz Prisons walio chini ya kocha mzoefu David Mwamwaja, wao wanacheza mchezo wa
pasi nyingi na hua wanawatumia wachezaji wao wa katikati, Jimy Shoji na Omega
Seme (inasemekana alikataa kucheza mchezo na Yanga, kwa vile tayari alikua
ameweka mkataba wa kuichezea timu hiyo msimu ujao) kupeleka mashambulizi mbele
ambapo wanamtegemea Peter Michael mwenye magoli zaidi ya nane msimu huu
kufunga. Pia wana beki wa kulia Salum Kimenya ambae ni mzuri sana wa
kupanda na kupiga krosi.
![]() |
| DAVID MWAMWAJA, KOCHA WA TZ PRISONS |
Timu zote zina walinzi wazuri sana wa katikati, Prisons yupo
Lugano Mwangama na Nurdin Chona ambao wanatumia akili na nguvu nyingi
kuwadhibiti washambuliaji wa timu pinzani, wakati Mbeya City wana uhakika na
mabeKi wao wa kati, Yohana Morris, Yusuf Abdallah pamoja na Deo Julius ambao
shughuli yao mara zote inakua ni kubwa na ya uhakika.
![]() |
| FRANCIS CASTRO WA MBEYA CITY AKIWAA NA JIMY SHOJI WA TZ PRISONS |
Kwa ujumla mchezo unatarajiwa kuwa wa ushindani zaidi,
hatutarajii kuona mchezo wa upande mmoja au wa kubebana, kwani kwa jinsi timu
hizi mbili zilivyo, kuna uadui mkubwa wa ndani ya uwanja ingawa mchezo ukiisha
wachezaji wengi ni marafiki. Ukitazama asilimia kubwa ya hawa wachezaji
wamecheza pamoja toka utotoni, wamkekuja kutengana tu pale wengine wanacheza
City na wengine Prisons.
Kwa
mashabiki wa timu hizo, tunategemea kutakua na kuzomeana, kutaniana na hata
kejeli za hapa na pale lakini hizo ndizo zinazofanya mchezo upendeze zaidi,
hatutegemei kutokea fujo kama zilizotokea walipokutana mzunguuko wa kwanza.
KILA LA KHERI TZ PRISONS NA MBEYA CITY.






No comments:
Post a Comment