Thursday, 6 March 2014

Taifa stars sare na Namibia

Timu ya soka ya Taifa Stars ya Tanzania, wametoka sare na Brave Warriors ya Namibia kwa kufungana goli moja kwa moja katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa.

       Tanzania walikuwa kwanza kupata bao baada ya beki wa Namibia Emilio Martin wakati wa jitihada za kuokoa  alijikuta akiusindikiza wavuni mpira wa kona iliyopigwa na Mcha Khamisi.

     Namibia walisawazisha goli hilo katika dakika za majeruhi kwa bao lililofungwa na Panduleni Nekundi.
     Stars ambayo  ilikwenda bila nyota wake wanaochezea timu ya Yanga na wale wanaocheza mpira wa kulipwa walionyesha mchezo mzuri na wa ushindani.

     

No comments:

Post a Comment