Sunday, 18 August 2013

               David Mwantika
       "HOME BOY"
                                 IMEANDIKWA NA ABDUL"be good"SUDI,MBEYA.
                                       PICHA KWA HISANI YA DAVID MWANTIKA


                                                              DAVID MWANTIKA
         
Sifa kubwa ya beki ni kutumia nguvu na akili,kucheza mipira ya juu na kuusoma mchezo.hivyo vyote  anavyo David Mwantika,ambae uhodari wake wa kutumia nguvu na akili umemfanya awe mmoja kati ya mabeki wazuri sana hapa Tanzania,ana uwezo wa kupiga miguu yote miwili,anajua sana kukaba,iwe man to man au hata kukaba nafasi,pia ni mzuri sana wa kutazama mashambulizi kabla hayajafika hivyo mara nyingi amekua akiwapanga wachezaji wenzake ili kuziba njia zote na kulifanya lango lao liwe salama.na kikubwa anachowazidi mabeki wengine ni kua ni mzuri sana kucheza mipira ya juu,hivyo ana uhakika wa asilimia nyingi wa kumlinda kipa wake.

                                   MWANTIKA AKIMDHIBITI SAID BAHANUZI  WA YANGA
      “Kucheza mpira si nguvu peke yake,na akili ina nafasi yake,hivyo kikubwa kinachotakiwa unapokua uwanjani ni kuwa makini muda wote wa mchezo,usiondoe mawazo mchezoni hata kwa sekunde moja kwani unapojisahau hapo hapo watu wanatumia nafasi na kuwaumiza”alinambia nilipoongea nae. “mifano ipo mingi,mnaweza kua mnacheza na kujiona kama tayari mmewazidi mmnaocheza nao,mnajiamini na hapo ndio kosa kubwa linapofanyika kwani nao wanakua wanajipanga wapate nafasi,mkikosea kidogo wanawapiga bao inakua kazi kuanza kutafuta la kurudisha”Alinifafanulia Mwantika aliyezaliwa mkoani Mbeya sehemu inayoitwa Ilomba,mbele kidogo ya kitongoji maarufu sana cha MWANJELWA ambacho kina pilika pilika nyingi mno za biashara.Alisoma elimu ya awali katika shule ya msingi Ilomba,ambapo ndipo alipoanzia kucheza soka “pale shuleni kulikua na ushindani sana wa soka,maana kama kukiwa hakuna kipindi kinachofanyika ni kuchukua mpira na kwenda kiwanjani,na huko ilikua ni mashindano maana timu mbili ndio zinashindana kila siku,na hakuna inayookubali kushindwa”alinieleza David ambae toka akiwa darasa la nne alikua akiichezea timu ya shule “nimecheza sana mashindano ya umitashumta,na wakati nipo shule nikawa nachukuliwa na timu moja ya mtaani ikijulikana kama  HOME BOYS na huko nilkutana na washikaji wengi sana wanaojua soka la nguvu,nikawa napambana kupata namba na pale ilinisaidia sana kwani nilianza kujifunza kuwa nikicheza vibaya sipangwi,nikawa najituma sana kufanya mazoezi na nikipata nafasi ya kucheza mechi nafanya kweli”aliniambia huku akitabasamu baada ya kuwakumbuka rafiki zake aliokua nao HOME BOYS…. “kulikua na mafundi sana pale HOME BOYS bahati mbaya hawakupata nafasi ya kucheza timu kubwa kwani nawakumbuka rafiki zangu kina GWAKISA,AMULIKE na hata mdogo wangu aliyeitwa ATU walikua wanajua sana mpira,ni mazingira mabovu ndio yamesababisha hadi wakapotea”aliongeza kwa masikitiko.
       Wakati akiwa HOME BOYS viongozi wa timu ya kijiweni ya Uyole Mbeya wakamuona na kumchukua. “KIJWENI nako niliikuta timu ina ushindani sana,lakini nilipigana hadi nikawa na namba ya kudumu,tukacheza ligi daraja la kwanza ingawa hatukufanikiwa kupanda lakini ilikua ni timu bora sana nako kulikua na mafundi ambao kila siku nazidi kushangaa kwa nini hawakuja kucheza ligi kubwa,mtu kama EZE,MTUMBA na hata MOI walikuwa wanajua sana soka tofauti na watu wengi naokutana nao huku wanachezea timu kubwa huku viwango vyao ni vya kawaida sana,lakini ndio maisha,kila mtu na alichopangiwa”akasisitiza.


                                 DAVID MWANTIKA AKIMZUIA FELIX  SUNZU  WA SIMBA 
         Alipotoka KIJIWENI akachukuliwa na timu ya POLISI Mbeya ambako hakukaa sana akaenda  PRISON ya Mbeya ikiwa katika ligi kuu ya Tanzania bara,na huko alifanya sana kazi na kufanikiwa kua na namba ya kudumu. “kule PRISON timu ilikua nzuri na tulikua tunafanya sana mazoezi hivyo tulikua tupo fit sana,tatizo kubwa mechi za nyUmbani zilikua zinatusumbua kutokana na mashabiki kugawanyika kila tunapocheza,inakua kama unacheza ugenini,hadi leo sijui sababu gani watu walikuwa hawataki tushinde wakati nao ni watu wa Mbeya,siwezi kuwasemea kwani wao wanajua sana sababu zao”
        Baada ya kucheza kwa misimu kadhaa ndipo alipochukuliwa na AZAM mbako yupo hadi sasa. “hapa  AZAM timu imetulia,tuko vizuri sana,hata ikitokea mechi tumepoteza tunajua ni bahati mbaya lakini kwa vipaji na uwezo tupo juu ya timu zote za Tanzania,msimu huu unaoanza tuna uhakika wa kufanya vizuri zaidi ya misimu iliyopita,labda yaanze tena mazengwe ya vilabu vinavyojiita vikubwa lakini kwa soka tu tuko vizuri mno”alinambia Mwantika ambae katika mechi ya kombe la shirikisho dhidi ya timu ya AFR ya Morocco alitolewa kwa kadi nyekundu kwa mazingira ya ajabu sana. “hadi leo nikitazama tape za ile mechi namshangaa refa kwa nini alinitoa nje maana ile ilikua ni shoulder to shoulder,nikamzidi nguvu,lakini ajabu nashangaa nikapewa kadi nyekundu,niliumia sana kwani pale ndipo mechi ilipoishia,maana kabla ya kadi nyekundu tulikua tumeshawashika……”alinambia Mwantika.


                                 DAVID MWANTIKA AKIMTOA NJIANI MRISHO NGASA
       David amepania sana kujituma kwa bidii zaidi ili waweze kutimiza lengo lao na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa Tanzania. “kwa jinsi timu yetu ilivyo nzur sasa hivi,na ukichukulia tumeshakaa muda mrefu pamoja hatuna sababu ya kutufanya tushindwe kuchukua ubingwa”alisema Mwantika anaemkubali sana mshambuliaji wa timu yake  Gaudence Mwaikimba.”tutapigana hadi dakika ya mwisho najua tutashinda”alimalizia …Huyu ndio David Mwantika……HOME BOY  aliyepigana kutoka Ilomba Mwanjelwa Mbeya hadi AZAM FC,na bado safari inaendelea....……





1 comment: