AMSHA AMSHA MBEYA CITY……
Waichapa Rhino 3-1
Timu ya Mbeya City imefanikiwa kupata ushindi mzuri ugenini baada ya
kuifunga timu ngumu ya Rhino ya Tabora magoli matatu kwa moja katika mchezo wa
ligi kuu ya Vodacom uliochezwa katika
uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mkoani Tabora.Katika mchezo huo Mbeya City
walianza kwa kasi na kupeleka mashambulizi mengi langoni mwa Rhino lakini
umahiri wa golikipa wa Rhino uliwazuia washambuliaji wa Mbeya City kupata magoli
mengi.magoli ya mbeya City yalifungwa na Jeremiah Juma,Alex Setth na la tatu
likafungwa na Peter Mapunda. Na katika mchezo mwingine wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania
Azam wamefanikiwa kuifunga Mgambo Shooting kwa magoli 2-0, magoli ya Azam yalifungwa na mchezaji
aliyepandishwa katika kikosi hicho Farid Maliki katika dakika ya 67 kufuata
pasi nzuri aliyopewa na Erasto Nyoni,na goli
la pili lillifungwa na Kipre Tcheche kwa
njia ya penati baada ya mshambulia ji wa Azam Farid kuangushwa ndani ya kumi na
nane.Nayo timu ya Mtibwa imewafunga Ruvu JKT kwa magoli 2-1,kwa magoli ya
haraka haraka yaliyofungwa na Juma Luzio dakika ya 3 ya mchezo baada ya kazi
nzuri ya mkongwe Shaaban Kisiga kuwapunguza mabeki wa JKT na kumpa pasi
mfungaji,goli la pili lilipatikana dakika mbili baadae baada ya Mtibwa kufanya
shambulizi kali langoni mwa JKT na Juma Luzio akafunga baada ya kupata pasi
toka kwa Abdallah Juma.goli la JKT lilifungwa na Salum Machaku baada ya kupiga
kona iliyokwenda moja kwa moja wavuni. Nayo JKT oljoro imetoka sare ya magoli
2-2 dhidi ya Ruvu Shooting.

No comments:
Post a Comment