Friday, 11 October 2013

TZ PRISON KUWAVAA SIMBA

                                                                                      TZ PRISON
Timu ya TZ Prison ya mbeya jumamosi inakutana na Simba katika ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara katika uwanja wa taifa jijini Dar es salaam.Katika mchezo huo Tz Prison wataingia huku wakiwa tayari na kumbukumbu ya kuwafunga timu ya  Mgambo shooting katka mechi yao ya mwisho huku Simba wakitoka sare na timu ya Ruvu shooting.Mechi hiyo inatarajiwa kua ngumu kwani timu ya Tz Prison katika mechi za karibuni imeonyesha kiwango kizuri tofauti na ilipokanza ligi,wakati Simba kila siku kiwango kinazidi kushuka hivyo kwa kiasi kikubwa Tz  Prison wanajiamini na wana uhakika wa kupata point zote tatu.Katika mechi tatu za mwisho timu ya Tz prison ilitoka sare mbili na Azam na Mtibwa kabla hawajawafunga Mgambo 1-0,wakat Simba ilitoka sare ya 2-2 na Mbeya City kisha ikaifunga Ruvu JKT 2-0 kabla haijatoka sare tena na Ruvu shooting kwa goli 1-1.Lakini imekua ikilalamikiwa sana na mashabiki wake kutokana na kiwango cha chini inachokionyesha pamoja na kushinda.,Mechi nyingine itakayochezwa kesho itawakutanisha Kagera Sugar na Yanga mjini Kagera.

                                KILA LA HERI TZ PRISON

No comments:

Post a Comment