Saturday, 26 October 2013

Arsenal  yaifunga  palace

Arsenal wameweza kufanikiwa kutanua uongozi wao baada ya kuwafunga Crystal Palace kwa magoli 2-0,   moja kwa njia ya penati na Mikel Arteta  katika dakika ya 47  baada ya Sergei Gnagby kuchezewa faulo katika eneo la hatari,  na la pili likafungwa na Olivier Giroud katika  dakika ya 87 kufutia krosi safi ya Aaron Ramsey.

               Matheu Flamini na Santi Carzola walirudi kutoka majeruhi ingawa Flamini alimudu kucheza wa dakika 10 tu na kutoka baada ya kuanza kuchechemea,  nafasi yake ikachukuliwa na Gnabry.
    Arsenal walitengeneza nafasi nyingi na wakafanikiwa kupata goli  dakika mbili  baada ya mapumziko baada ya  Gnabry kuangushwa na Guedioura na Arteta kufunga kwa penati.


               Dakika ya 65 Arteta alionyeshwa kadi nyekundu baada ya kumvuta Maroune Charmakh aliyekua akienda kumuona golikipa, baada ya hapo hali ya mchezo ikabadilika kwani Palace walianza kushambulia na kutafuta goli la kusawazisha,lakini kipa wa Arsenal Szczesny aliokoa  mpira wa Joe Ward uliokua ukienda pembeni mwa goli na baadae akaokoa tena mpira uliopigwa na Mile Jedinaks.

          Olivier Giroud akaihakikishia Arsenal ushindi baada a kuunganisha krosi iliyopigwa na Ramsey na kumaliza ndoto za Palace za kusawazisha.
     Kwa ushindi huo Arsenal wamefikisha pointi 22 na kuzidi kujichimbia kileleni wakifuatiwa na Chelsea wenye point 17.

      

No comments:

Post a Comment