Friday, 25 October 2013

toure ataka waafrika kususia kombe la dunia


            Kiungo wa Manchestar City na Ivory Coast Yaya Toure amesema endapo UEFA  hawataichukulia hatua zinazostahili timu ya CSKA Moscow,nchi za Africa huenda zikasusia kombe la dunia la mwaka 2018 litakalofanyika Urusi. Toure aliyasema hayo mara baada ya viongozi wa soka nchini Urusi kukana kwamba hakukua na tukio la kumdhalilisha Toure au mchezaji yeyote mwenye asili ya Africa jambo ambalo limepingwa vikali na kiungo huyo.  “mimi sio kiziwi na mara kadhaa  nilimwambia mwamuzi kuwa natukanwa lakini hakuchukua uamuzi wowote kuzuia hali hiyo”alisema Toure.
WACHEZAJI WAKIMTULIZA TORE
                    Hivi karibuni shirikisho la soka ulimwenguni lilitangaza hatua za kuchukuliwa  endapo hali kama hii itatokea na ikaamuliwa mwamuzi analazimika kumaliza mchezo pindi akisikia  udhalilishaji kama huo.Raisi wa UEFA Michel Platini anasema anashangaa kwa nini mwamuzi kutoka Romania Ovidiu Hategan hakusimamisha mchezo hali hiyo ilipojitokeza na kusema uchunguzi tayari umeanza kufanyika na hatua kali zitachukuliwa kwa timu hiyo ya Urusi.
YAYA TOURE
                   Kumekua na ongezeko kubwa la udhalilishaji wa waafrika na hali inazidi kua mbaya kwani adhabu zinazotolewa zinakua ni ndogo sana kufananisha na kosa lenyewe. Klabu zinakua zinatozwa faini ndogo kiasi inakua kama vile hawajaadhibiwa.
          Katika hali ya kushangaza,mchezaji anayechezea timu hiyo ya  CSKA Moscow na raia wa Ivory Coast kama toure, Seydou Doumbia mwanzo alikaririwa akisema hakusikia milio kama ya nyani au matusi yoyote yakielekezwa kwa Toure au mwafrika yeyote,lakini baadae alikana akasema hajawahi kuongea na mwandishi yeyote juu ya jambo hilo kwa hiyo hajasema hayo maneno.Yaya Toure kwa upande wake alisema anamuheshimu sana Doumba na anajua kama aliyasema hayo maneno ni kwa sababu ya kulazimishwa na klabu yake na sio kutoka moyoni.Mchezaji mwenzake wa Manchester City Fernandinho alisema kama hali hii itaendelea na yeye atakua sambamba na waafrika kususia kombe  la dunia litakalofanyika Urusi,kwani ni jambo lisilopendeza na linakera.
SEYDOU DEMBA
             Nae kocha wa Chelsea Jose Mourinho amesema kususia sio suluhisho kwani wanaofanya hivyo ni wachache sana na wanaopinga ni wengi ni bora zikachukuliwa hatua za haraka ili kuokoa,  kwani  kombe la dunia bila waafrika litakua si kombe la dunia tena hivyo haitakiwi wakasusa bali hatua zichukuliwe haraka kukomesha hali hiyo.

No comments:

Post a Comment