Man utd
yashinda kwa tabu
Man united wamefunga magoli mawili ya haraka
haraka na kunusurika na kipigo toka kwa Stoke City waliokua wakiongoza kwa
magoli 2-1 hadi zikiwa zimesalia dakika 12,lakini magoli ya Rooney na
Chicharito yalisaidia kupata ushindi huo.
 |
| PETER CROWCH AKISHANGILIA GOLI LA KWANZA |
Stoke City walikua wa kwanza kupata
goli katika dakika ya nne tu baada ya kipa wa
United De Gea kuokoa mpira uliopigwa na Peter Crowch lakini wakati Evans
akijaribu kuosha ukamgonga tena Crowch na kuandika goli la kwanza.
De Gea alikua tena shujaa baada
ya kuokoa michomo kadhaa kabla ya dakika ya
44 Robin Van Persie hajasawazisha kutokana na kichwa kilichopigwa na
Wayne Rooney kuokolewa na Asmir Begovic na kumkuta Van Persie aliyeukwamisha wavuni.
 |
| VAN PERSIE AKISHANGILIA GOLI LA KUSAWAZISHA |
Lakini
kabla hawajatulia, Stoke wakaongeza goli kwa faulo iliyopigwa na Marko Arnautovic
na kufanya timu hizo kwenda mapumziko Stoke ikaenda kifua mbele kwa magoli 2-1.
 |
| MARKO ARNAUTOVIC AKIFUNGA KWA FAULO GOLI LA PILI |
Man
wakashambulia sana kipindi cha pili,hasa alipoingia Adnan Januzaj kuchukua
nafasi ya Nani, alibadilisha kabisa hali ya mchezo kwani waliwasumbua vilivyo
Stoke na kufanikiwa kusawazisha zikiwa zimesalia dakika 12 baada ya kona ya Van
Persie kumkuta Wayne Rooney akaukwamisha
wavuni.
 |
| ROONEY AKISAWAZISHA GOLI LA PILI |
Dakika mbili baadae
Chicharito aliyeinga kipindi cha pili kuchukua nafasi ya cleverly alimalizia
vizuri krosi iliyopigwa na Patrice Evra na kuandika bao la tatu na la ushindi.
 |
| CHICHARITO AKIFUNGA GOLI LA TATU NA LA USHINDI |
Mabadiliko yaliyofanywa na Man United ya kuwaingiza januzaj na Chicharito yalisaidia sana kuleta uhai kwa timu hiyo na kuepuka janga la kufungwa nyumbani.
No comments:
Post a Comment