Monday, 28 October 2013

Azam yaitoa nishai simba

           Azam imeweza kutumia udhaifu wa timu ya Simba na kuweza kuwashinda kwa magoli 2-1,  katika  mchezo mzuri wa ligi kuu ya Vodacom Tanzania bara uliochezwa katika uwanja wa taifa Dar es salaam.
              Hadi kipindi cha kwanza kinakwisha timu hizo zilikua zmefungana goli moja kwa moja.Simba ilikua ya kwanza kupata bao lililofungwa na Ramadhani Singano baada ya kazi nzuri iliyofanywa na kiungo wa kati wa Simba Said Ndemla kupiga pasi ya pembeni iliyomkuta  Zahor Pazi aliyempita kirahisi beki wa kushoto wa Azam Wazir Seif na kupiga krosi  ndogo iliyomkuta  Singano aliyewahamisha mabeki wa Azam na kupiga shuti lililopita kushoto mwa goli la Simba na kuandika goli la kwanza.
ZAHORO PAZI AKIKIMBIA KUSHANGILIA BAADA YA KUTOA PASI YA GOLI LA KWANZA LA SIMBA
      Azam hawakutetereka na goli hilo kwani walifanya shambulizi kubwa na pasi ndefu ya Abubakar Salum ilimkuta John Boko aliyemzidi nguvu beki wa Simba Hassan Hatibu na kupiga shuti lililotoka nje.
          Simba ilikua ikifanya mashambulizi mengi kupitia kwa Singano ambae mara kwa mara alikua akimsumbua Said Morad na dakika ya 34  alipiga pasi  nzuri iliyomkuta Zahor Pazi aliyeingia nao katika eneo la hatari na alippotaka kupiga aliwahiwa na Agrey Moris na kua kona ambayo haikuzaa matunda.
WACHEZAJI WA SIMBA WAKISHINGILIA GOLI LAO

           Azam walisawazisha kutokana na mpira uliotoka katikati ya uwanja  na Kipre Balou alipiga pasi upande wa kulia mwa uwanja ukamkuta Abubakar aiyempigia pasi  Erasto Nyoni ambae alimaliza uwanja na kupiga pasi nzuri iliyomkta Kipre Tcheche aliyeukwamisha wavuni.
            Kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko  kwa kumtoa Zahor Pazi na Amri Kiemba na nafasi zao kuchukuliwa na Christopher Edward na Sino Augustino wakati Azam walimtoa Said Morad na Josef Kimwaga na kuwaingiza David Mwantika na Malick mabadiliko yaliyowasaidia sana Azam, kwani Mwantika aliweza kumzuia Singano vizuri na kuziba njia zote za kupenyeza mipira.
RAMADHANI SINGANO AKIJIPANGA KUMTOKA SAID MORAD
        Azam walipata bao la pili kupitia tena kwa Kipre Tcheche  aliyepigiwa pasi ndefu na Abubakar Salum na kumpita kirahisi Wiliam Lucien na kuupiga mpira kiufundi na kupita pembeni mwa lango la Simba na kuandika bao la pili.
       Simba walipata nafasi ya kuswazisha goli hilo baada ya Mombeki kumpigia pasi nzuri Sino lakini akashindwa kufunga.
SINO AUGUSTINO,SURE BOY,MWANTIKA NA PEMBENI BALOU WAKIMPITA CHISTOFER EDWARD ALIYEUMIA
 Kwa ujumla  Simba hawakucheza vizuri kabsa katika mchezo wa huo  kwani mabeki wake wa kati  Owino na Hassan Hatibu walikua hawaelewani mara kwa mara na hata Wiliam Lucien aliyecheza kama beki wa kulia alisumbuliwa sana na Kipre Tcheche, hadi sasa timu ya Simba bado haijapata kikosi cha kwanza  na hilo linawasumbua sana.     
KOCHA WA AZAM AKIONGEA NA CAPTAI WA SIMBA KATIKA MECHI HIYO, OWINO
            

                     Na hata mabadiliko waliyofanya hayakuwasaidia sana lakini Azam walifanya mabadiliko na yalisaidia kuongeza nguvu na ufundi hadi wakafanikiwa kupata ushindi.

No comments:

Post a Comment