Sunday, 27 October 2013

Torres awamaliza man city

        Fernando Torres ameweza kusaidia kutoa pasi ya goli la kwanza na kufunga la pili na kuiwezesha timu yake ya Chelsea kuifunga Man City kwa magoli 2-1.

        Katika mchezo huo ambao ulikua mgumu na kila mmoja akitarajia kuwa utaisha kwa sare ya goli 1-1 Torres alitumia vizuri makosa yaliyofanywa na beki wa City Matija Natascic na kipa wake Joe Hart kuchanganyana  na mpira kumkuta Torres aliyefunga kirahisi.
             Aguero aliisawazishia  City baada ya kupata pasi nzuri toka kwa  Samir Nasri na akapiga mpira uliokwenda pembeni mwa goli na kuandika goli.

   Goli hilo liliwafanya Man City kuendelea kushambulia na Aguero alikosa tena goli la wazi pale mabeki wa Chelsea walipodhani ameotea lakini alipojaribu kuubetua mpira ukatoka nje. Na shuti kali la Ramirez aliyekua akihaha uwanja mzima lilitoka nje idogo ya goli la City.


     Gary Cayhil nusura aipatie timu yake goli lakini alipobaki na kipa wa City Joe Hart,  aliupaisha mpira kwa mshangao wa wengi.

                       Torres aliyecheza vizuri sana katika mchezo huo aliweza kuipa ushindi timu yake alipofunga dakika ya tisini ya mcezo na kuifanya itoke uwanjani kwa ushind wa 2-1.

                Kocha wa Chelsea alishindwa kujizuia kwa furaha na kukimbia had kwa masahbiki wa timu hiyo na kushangilia pamoja nao..

No comments:

Post a Comment