mbeya city yashinda
Mbeya derby
NA ABDUL SUDI,MBEYA
Mbeya derby
NA ABDUL SUDI,MBEYA
Timu ya Mbeya City imefanikiwa
kutoka na ushindi mnono wa magoli 2-0 dhidi ya wapinzani wao wakubwa timu
ya Tz Prisons ya hapo hapo jijini Mbeya, katika mchezo mkali uliojaa kila aina ya
ufundi.
Katika mchezo huo, muamuzi Israel Mkongo toka Dar es salaam
alimudu vilivyo na kusifiwa na mashabiki waliotazama mchezo huo.
![]() |
| ISRAEL MKONGO |
Hadi timu hizo zinakwenda
mapumziko zilikua bado hazijafungana ingawa kosa kosa zilikua nyingi kwa kila
timu.
![]() |
| KOCHA WA MBEYA CITY JUMA MWAMBUSI |
Prison ndio walioanza kutawala dakika za
mwanzo kwani walifanya mashmbulizi mengi ingawa safu ya ulinzi ya Mbeya City
iliyokua ikiongozwa na Yusuph Abdallah
na Deoratius Julius walifanya kazi nzuri ya kuwazuia washambuliaji wa Prison na
hasa Peter Michael aliyekua akiwasumbua
mara kwa mara.
![]() |
| MBEYA CITY |
Nao Mbeya City walizinduka na
Alex Seth alifanya kazi nzuri mara kadhaa ya kuwatoka mabeki wa Tz Prisons na
kupiga krosiambazo zilikkua zikiokolewa.
Kipindi cha pili Prison walianza tena
kwa kasi na kukosa goli la kuongoza baada ya kufanya shambulizi kali na mpira
uliookolewa na mabeki wa Prison ulimkuta Peter Mapunda aliyepiga shuti kali na
kuandika goli la kwanza.
![]() |
| TZ PRISONS |
Mbeya City waliendelea kushambulia
na kufanikiwa kupata bao la pili lililofungwa kwa njia ya penati baada ya beki
wa Prison kumfanyia madhambi shambuliaji wa Mbeya City Deus Kaseke,na Deogratus
Julius akafunga penati hiyo.
![]() |
| WACHEZAJI WA MBEYA CITY WAKISHANGILIA GOLI LA KWANZA |
Kwa kiasi kikubwa mabadiliko
yaliyofanywa na kocha wa Mbeya City Juma Mwambusi ya kumbadilisha Jeremiah John
aliyeumia na nafasi yake kuchukuliwa na Mwagane Yeya,na kkumtoa chipukizi Alex
Seth na nafasi yake kuingia Peter Mapunda ndio yaliyobadilisha kabisa hali ya
mchezo huo, kwani mashambulizi yaliongezeka na kufanikiwa kupata mabao yote
mawili.






No comments:
Post a Comment