Saturday, 26 October 2013


Real yatota kwa barca

Magoli yaliyofungwa na Neymar na Alexis  yaliwafanya Barcelona kutoka na ushindi mzuri wa magoli 2-1 dhidi ya wapinzani wao wakubwa Real Madrid.
          Barcelona walikua wa kwanza kupata bao katika dakika ya 19 lililofungwa na Neymar baada ya kupokea pasi toka kwa Andres Iniesta.
 Real walishambulia sana ii kupata bao la kusawazisha lakini kipa wa Barcelona alikua imara na kuzuia micho ya Khedira na Ronaldo waliokuwa na uchu wa kufunga.

      Real waliendelea kushambulia na Ronaldo alingushwa katika box la penati lakini mwamuzi hakutoa penati na baadae Benzema alipiga shuti likagonga mwamba.

                    Zikiwa zimesalia daika 12 mpira kumalizika  Barcelona walipata bao lililofungwa na Alexis Sanchez na kumaliza kabisa matumaini ya Real kusawazisha.


         Goli la kufutia machozi la Real lilipatikana katika dakika za nyongeza likifungwa na Jesse baada ya kupokea mpira toka kwa Ronaldo.
       Kiungo  Gareth Bale hakuonyesha makeke yake zaidi ya kupiga shuti kali lililotoka nje na baadae kupewa kadi ya njano kwa mchezo mbaya.   Alitolewa katika dakika ya 60 na nafasi yake ikachukuliwa na Karim Benzama aliyeongeza uhai katika timu yake.

No comments:

Post a Comment