Saturday, 5 October 2013

MBEYACITY YAICHAPA OLJORO  2-1

                                                mbeya city
Timu  ya Mbeya City imefanikiwa kuifunga timu ya JKT Oljoro ya Arusha kwa magoli mawili kwa moja katika mchezo mkali na mzuri uliochezwa katika uwanja wa sheikh Amri Abeid Arusha.City ndio waliokuwa  wa kwanza kupata bao lililofungwa na mshambuliaji hatari Mwagane Yeya baaada ya krosi safi iliyopigwa toka kushoto mwa uwanja na mpira ukamkuta Paul Nonga aliyepiga shuti kali lililomshinda kipa wa Oljoro na mpira ukawa unaelekea golini  na ndipo mwagane akaumalizia na kuandika goli la kwanza.City walikitawala kipindi cha kwanza na hadi mapumziko goli likawa hilo moja.kipindi cha pili Oljoro waliingia kwa nguvu na kufanya mashambulizi mengi kuelekea kwa City,na uhodari wa mabeki wa City wakiongozwa na Yohana Morris na kipa Baruan walikua makini na kuweza kkuzuia mashambulizi hayo.City wallipata bao la pili kwa counter attack baada ya Oljoro kufanya shambulizi kali golini mwa City na ndipo kipa wa City Baruan alipodaka akapiga mpira mrefu uiomkuta Peter Mapunda aliyekua katikati ya mabeki wawili na kufanikiwa kuwapita na kukimbia mbele kidogo na kupiga shuti kali lililomshinda kia wa Oljoro na kuandika goli la pili.ni moja kati ya magoli mazuri sana yaliyofungwa katika ligi ya mwaka huu.Oljoro walipata goli lao kipindi ch pili baada ya kufanya mashambulizi mengi na kufanikiwa kupata bao hilo,hadi mwisho JKT Oljoro 1 na Mbeya City 2 WELL DONE MBEYA CITY

No comments:

Post a Comment