Friday, 18 October 2013

Mbeya city uso kwa uso na jkt ruvu
                                                                                      NA ABDUL SUDI


                                                                             SHABIKI WA MBEYA CITY
Timu ya Mbeya city iliyo katika form kali,jumamosi inapambana naJKT ruvu katika mfululizo wa michezo ya ligi kuu ya Vodacom Tanzania.Katika michezo yake iliyopita Ruvu stars ilifungwa magoli 3-0 na Azam na kabla ya hapo walikua wamefungwa naSimba2-0,kisha na Mtibwa 2-1 hivyo watakua wanatafuta kwa nguvu sana ushindi ili uweza kujiweka katika nafasi nzuri.
                   Mbeya city wana kumbukumbu nzuri ya ushindi mfululizo katika michezo yake kwani katika michezo mitatu iliyocheza ugenini  imefanikiwa kujipatiapoint zote tisa kwakuwafunga JKT Oljoro 2-1mjini Arusha,kisha wakawafunga Rhino yaTabora 3-1na mwisho wamewafunga  Mgambo JKT kwagoli 1-0.Hivyo wako ktika kiwango kizuri na ukichukulia wanacheza katika uwanaja wao wa nyumbani ulio na sifa ya kujaza mashabiki wake wanaoisapoti timu hiyo kwa kuishangilia mwanzo hadi mwisho.
                Akielezea mchezo huo,kocha wa timu ya Mbeaya City Juma Mwambusi amesema wanauchukulia kwa tahadhari kubwa sana mchezo huo kwani kwa vile wameshashinda mechi  tatu mfululizo wanajua wapinzani wao watakua wamejipanga vilivyo kujilinda  na kufanya mashambulizi ya kushtukiza,hivyo amewaambia vijana wake watashambulia mwanzo hadi mwisho ili wawezekuondoka na point tatu muhimu katika mchezo huo,aliongeza hadi sasa timu iko vizuri na hakuna majeruhi wa kutisha katika timu hiyo,hivyo wapenzi na mashabiki wa soka jijini hapa wategemee mchezo mzuri na Insha allah timu itashinda.

         Michezo mingine inayotarajiwa kuchezwa mwisho wa wiki hii ni  Kagera sugar watawakaribisha Coastal Union,JKT Oljoro watacheza  Azam,wakati Mtibwa sugar watakua wenyeji wa Mgambo shooting,na Ashanti watacheza na Ruvu Shooting.jumapili ni Simbana Yanga.

No comments:

Post a Comment