Saturday, 19 October 2013

 USIOMBE KUKUTANA NA
MBEYA CITY,ni BALAA….
     NA ABDUL SUDI,MBEYA

                                                                         wahamasishaji wa mbeya city
MBEYA CITY leo katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine imeendeleza wimbi la ushindi baada ya kuifunga timu ya JKT  stars kwa goli 1-0 katika lig kuu ya Vodacom Tanzania bara,huu ni mchezo wa nne mfululizo kwa timu hiyo kushinda baada ya kuzifunga timu za Oljoro JKT 2-1,Rhino Rangers 3-1,kisha kuwafunga Mgambo JKT 1-0 na sasa kuwafunga JKT Stars 1-0.
         Goli la ushindi kwa Mbeya City lililofungwa na mshambuliaji wake hatari Jeremiah John katika dakika ya 30 ya mchezo baada ya kona iliyookolewa na walinzi wa JKT na mpira kumkuta mfungaji aliyepiga shuti kali lililotinga wavuni.
           Mbeya City itajilaumu kwa kukosa magoli mengi ya wazi hasa kipindi cha pili kwani waliutawala mno mchezo na kushinda golini mwa JKT lakini uhodar wa kipa na kutokua makini kwa washambuliaji wake kuliifanya timu hiyo kumaliza mchezo na goli hilo hilo moja,
            Kocha wa timu hiyo Juma Mwambusi  kama kawaida aliwashukuru sana mashabiki wa timu hiyo kwa kuwapa sapoti kubwa na pia aliwashukuru wachezaji wake kwa kujituma na kuweza kufanikisha ushindi huo.
           Kwa ushindi huo timu ya Mbeya City imefikisha pointi  20 sawa na Azam na kuongoza ligi hiyo kwa muda.

                                                        KIVYETU VYETU
 Na katika mchezo mwingine wa ligi hiyo,timu ya Mtibwa imeifunga  Mgambo JKT kwa magoli 4-1 mchezo uliochezwa  katika uwanja wa manungu.magoli ya Mtibwa yalifungwa na Shaaban Nditi aliyeunganisha kwa kichwa kona ya Awadh  Juma  ,na goli la pili lilifungwa na mchezaji chipukizi  Juma Luzio baada ya kupata pasi ya shaaban nditi,na goli la tatu lilifungwa tena na  Juma Luzio  baada ya kupata mpira katikati ya uwanja na kuwapita mabeki wa mgambo  kisha akakimbia  na kupiga shuti kali la mguu wa kushoto lililomshinda kipa wa Mgambo Kaviche  na kuingia.Goli la nne lilifungwa na Shaaban  Mkopi.Mgambo walikuja kupata goli la kufutia machozi kupitia kwa   Nguya dakika ya 83 kwa njia ya penati baada ya mshambuliaji wake kuangushwa katika eneo la hatari.      
Nayo timu ya Kagera  Sugar imefanikiwa kuifunga timu ya Coastal Union ya Tanga kwa goli moja lililofungwa na Salum Kanon kanon  dakika  ya 60 kwa njia ya  penati.         
Azam wameifunga JKT Oljoro ya Arusha  goli moja liliofungwa na kiungo wake Mcha Khamis katika dakika ya 67.


   Nayo Ashanti imelazimisha sare ya magoli 2-2 na timu ya Ruvu Shooting katika mchezo uliochezwa uwanja wa AZAM,Ruvu ilikua ya kwanza kupata magoli yake yote mawili moja kila kipindi yaliyofungwa na lakini Ashanti walikuja kuzinduka dakika 20 za mwsho na kufanikiwa kusawaziha magoli yote mawili.

No comments:

Post a Comment