Monday, 14 October 2013

OZIL
 Atabiriwa kuwapa
arsenal ubingwa

Kiungo wa timu ya Arsenal Saint Carzola anaamini ujio wa mtaalam Mersut Ozil katika klabu hiyo umewapa hamasa wachezai wengine kupigania ubingwa na kumaliza ukame wa makombe.
          Kocha wa Arsenal,Arsene Wenger alivunja rekodi za gharama za usajili wa timu hiyo baada ya kumchukua Ozil kutoka Real Madrid dakika za mwisho za dirisha dogo la usajili ka gharama ya paundi milioni 42.
           Carzola anasema bado anashangaa kwa nini Real Madrid walimuachia mchezaji mwenye kiwango bora kama cha Ozil na alifurahi sana kumuona akijiunga na Arsenal.

      “nilishangaa sana kusikia Madrid  wanamuacha na nilifurahia mno kuona mchezaji mwenye kiwango kama chake anakuja kucheza na sisi,na alipokuja hakua na makeke yoyote,alikuja na kuanza kufaya kazi mara moja,ni mchezaji ambae unajifunza mengi sana toka kwake,na ni mtaalamu sana”alisema Carzola.
           Akimuongelea Ozil mshambuliaji wa zamani wa timu hiyo Robert Pires amesema “Ozil ameleta kitu ambacho kilikua kinahitajika muda mrefu sana,Arsenal wamezoeleka kwa kukaa sana na mipira lakini hawako makini kwa kutoa pasi za mwisho lakini sasa amekuja Ozil anaifanya hiyo kazi na kuwarahisishia wengine kufunga kirahsi,hadi sasa tayari kafunga na kutoa pasi tatu za magoli,ni kiwango kizuri sana  

          Kocha Arsene Wenger yeye anasema  kuja kwa Ozil kumeamsha ari kwa wachezaji wengine wa Arsenal,ni usajili sahihi ambao malio yake yankuja pale pale bil kusubiri muda.
    Ozil alicheza michezo 105 akiwa Werder Bremen na kufunga magoli 16 n kutoa pasi za mwisho 55,alipokwenda Real Madrid alifunga magoli 27 akatoa pasi 81 katika michezo 159 na kumfanya awe ni kiungo mshambuliaji bora  katika ligi zote za ulaya kwa msimu uliopita.na wengi wanaamini alikua ni kiungo mshambuliaji bora duniani msimu uliopita.


No comments:

Post a Comment