Friday, 25 October 2013

OSCAR… kiungo
 chelsea

               NI mzuri sana kwa kupiga shuti  akitumia pembeni mwa mguu (outer), anapiga chenga za haraka sana bila kufikiria kwa muda mrefu,  na anajua ni muda gani apige shuti hata akiwa mbali na goli,mara nyingi anafanikiwa kupata magoli na yanakua mazuri sana. Wengi walikua wakimfananisha na Kaka kwa jinsi anavyomudu kugawa mipira akiwa kama kiungo wa juu,  lakini ameonyesha ana uwezo hata wa kua mshambuliaji kani mara nyingi mpira unapofika katika penat box nae tayari anakua kafika.

           Oscar alizaliwa mwaka 1991  na alianza kucheza mpira katika timu ya Sao Paolo mwaka 2008, lakini mwaka 2009 aliipeleka mahakamani timu hiyo baada ya kukiuka makubaliano ya mkataba waliokuwa wameweka. Baada ya hapo alihamia timu ya Internacional alikokaa miaka mitatu hadi alipohamia Chelsea.

           Akiongelea kipajichake anasema ni kitu alichokirithi toka kwa baba yake ambae ingawa alikua na kiwango kikubwa sana lakini mazingira yalimzuia kufika mbali zaidi na pia mjombake ambae nae kama baba yake hakufika mbali ingawa alikua na kipaji.Baba yake alifariki Oscar akiwa na miaka mitatu hivyo hakuweza kumuona mwanae akiwa ni mmoja a nyota wa soka duniani.

                 “ingawa baba yangu hayupo duniani lakini nina furaha kwamba angalau mjomba yupo na anafatilia sana maendeleo yangu kwani kila nikicheza mechi lazima niikute message zake katika simu akinipongeza na kunikosoa kwa kila ninalofanya uwanjani,hua nazisubiri kwa hamu message zake na za binamu zangu,hua zinanipa faraja sana na kuiona nawakilisha familia duniani”alinukuliwa Oscar. “natamani sana kama bba yangu angekuwepo,lakini ndio hali ya dunia,huwezi kuhindana nayo,kilichopo ni kua nafanya vizuri na malengo aliyokua nayo wakati kijana mimi nayatimiza,na ninajitahidi sana kufika mbali zaidya hapa”alisema Oscar.

                         Kwa sasa Oscar amekua ni tegemeo la timu ya Chelsea kwani mara nyingi anacheza kama kiungo wa mbele,anagawa mipira na anafunga magoli muhimu kila akipata nafasi.


No comments:

Post a Comment