Friday, 25 October 2013


 

 

          

PRODUCER EPHRAIM KAMETA                           
 Wengi wamemjua Ephraim Kameta baada ya kumtoa msanii maarufu sana wa bongo flava,   Mr nice lakini Kameta hakuanza leo kufanya shughuli za muziki, kwani wakati bado mdogo kabisa mwaka 1984 alikua akipiga na wakongwe kama marehemu Patric Balisidya na Ludala katika bendi iliyokua ikijulikana kama African Roots,na hata katika ule mwimbo maarufu sana wa bendi hiyo wa JIRANI, Kameta ndie aliyepiga lead guitar.  “nilifurahia sana kufanya kazi pamoja na mtu kama Patric Balisidya kwani uzoefu wake tu katika muziki ni shule tosha,maana alikua anajua sana muziki.”
KAMETA AKIWA NA TUZO ZAKE

    Kameta alizaliwa mkoani Mbeya eneo la soko matola   na kupata elimu yake mkoani humo humo akianzia na elimu ya msingi katika shule ya Majengo na kumalizia katika shule ya mbeya primary ambayo kwa sasa ipo shule ya Meta.  Alijifunza kupiga muziki kanisani, kanisa la ASSEMBLIES OF GOD ambalo baba yake alikua ni mchungaji na walikua wakiishi jirani na hilo kanisa, alianza kugusa chombo kimoja kimoja na matokeo yake akaja kuwa mtaalamu wa kupiga kila aina ya zana.   “Nilipopata tu urefu wa kukaa katika kiti na kuifikia organ,nikaanza kujifunza kupiga organ,  baadae akaja mpiga gita mmoja akiitwa John, nikatokea kuhusudu sana upigaji wake, nae akanisogeza na kuanza kunifundisha kupiga gita,  na kuna wakati yalikuja mahubiri makubwa pale kanisani na siku hiyo watu wakamshangilia sana mpiga gita la besi hapo nikatamani sana na mimi niwe mpiga besi,nikamfata nae hakua mchoyo akanifundisha…matokeo yake ikawa kila akichelewa mpigaji wa chombo chochote naitwa na kuziba nafasi yake,na sikuwaangusha kwani nilikua napiga vizuri kiasi hakuna aliyewahi kugundua kama mimi si mpigai rasmi”  alinisimulia huku akicheka.
                Mwaka 1984 akahamia Dar, na huko ndipo akakut
AKIWA NA FAMILIA

ana na wataalamu kama kina Patric Balisidya na bendi ya African Roots na kurekodi nao nyimbo kadhaa kisha akarudi tena Mbeya,  akajiunga na bendi ya MIONZI ambako alikutana na wanamuziki maarufu wakati huo kina Martin aliyekua akipiga kinanda na mdogo wake Deric aliyekua akiimba, pia walikuwepo kina Noel.  Lakini baadae mwaka 1994 akarudi tena Dar na kujiunga na bendi ya INAFRICA akiwa na kina ras Pompi pamoja na Enrico. Na hapo pia alirikodi nyimbo kadhaa kabla hajaenda kuanzisha bendi ya OLDUVAI akiwa na kina Noel na Issa na hapo walifanikiwa kurekodi nyimbo nyingi lakini mojawapo iliyokua maarufu zaidi ni ‘baba kaleta panya’
     “Mwaka 1999 nilipata nafasi ya kwenda Germany katika kozi ya muziki,na nilisoma kwa mwaka mmoja na kupata diploma ya kutayarisha muziki na niliporudi mwaka 2000 ndio nikaamua kuanzisha  kampuni yangu ya production ya AK PRODUCTION,”alisema Kameta   “Nilipoanza production nikapata watu kadhaa wa kuwatengenezea nyimbo zao,na ukweli zilikua zinafanya vizuri sana,    kuna muda nilifanya kazi na watu ambao hata hawajawahi kufikiria kua siku moja watakua wanamuziki,na kazi zao nilipomaliza zikawa nzuri kiasi hata wenyewe walishangaa walipozisikia mara ya kwanza,Mtu kama Bambo alipokuja na wazo lake la kutoa mwimbo wa KITAMBI,hakuna aliyedhani kama utakua mzuri,lakini tukakaa chini na kuufanyia kazi matokeo yake wote mmeona,  hata King’wendu nae tulifanya nae kazi ya kuutengeneza mwimbo wa MAPEPE,  ingawa inakua ngumu sana kufanya nao kazi, lakini ukidhamiria inalipa,nao ukaja kua ni hit sana,kila mtoto anaujua MAPEPE….”
FAMILIA
             Akiongelea kuhusu kazi ambazo aliumiza sana kichwa kuzitengeneza,KAMETA ambae sasa hivi ana kampuni inayoitwa TIKA PRODUCTION hakosi kukuambia kuhusu albam mbili aliomfanyia MR NICE    “Unajua mwaka 2001/02 mimi ndie nilimfanya mr nice atoke,  sababu albam zake zote mbili nilitoa mimi,na nilikua naumiza sana kichwa,  sio siri MR NICE ni mzuri sana wa kuimba lakini inatakiwa uujue sana muziki ili umfanyie kazi zake,  kwangu mimi nasema,hata leo MR NICE akija kwangu, atarudi kule kule juu alikokua, sababu mimi ni mwanamuziki na najua anachohitaji,  najua mapungufu yake na pia tayari tulikwishajuana , hivyo ni rahisi sana kumtengenezea kazi na ikamtoa tena”      alipoulizwa  kwa nini walitengana kikazi na MR NICE alinijibu kifupi sana    “alipopata mafanikio akapata pia na washauri wabaya, hivyo tukashindana, na hilo limetokea si kwake tu bali kwa wanamuziki wengi,  unaumiza kichwa kwa kumuona ana talent lakini akitoa mwimbo mmoja  tu na kua hit, anakimbilia kwa maproducer wao waliojifunza kutengeneza muziki kwa computer, baadae ana flop anaanza kuhangaika,  wapo wengi sana wa aina hiyo”
STUDIO
          Kameta kawatoa watu wengi sana.wanamuziki kama MEZ B na mwimbo wake wa KIKUKU mwaka 2002,  wakati mwaka 2003 akamtoa SUPER DANGER na hit yake ya UTANIKUMBUKA,  pia mwaka 2004 akamtoa RICHIE RICH na mwimbo wa FUNGUO..   wote hao alifanya nao kazi zilizokuja kua hit sana kwa miaka hiyo.  Hata wanaoimba nyimbo za dini pia kafanya Kazi na wasanii wengi sana maana mwaka 2005 alifanya kazi na BIG NOVEMBER CRUSADE na wakatoa mwimbo wa SIPATI PICHA,  akafanya na mwanamuziki maarufu sana hapa Tanzania,  BONIFACE MWAITEGE wakatoa mwimbo ambao hadi leo bado ni hit wa UTANITAMBUAJE KAMA NIMEOKOKA,  akaja kumtengenezea tena mwanamuziki AMBWENE mwimbo wake wa MAJARIBU NI MTAJI,  pia  NEEMA MWAIPOPO na mwimbo wake wa RAHA JIPE MWENYEWE pia aliufanya KAMETA.baadae akaja kumtengenezea BONY mwimbo wa MAMA,kisha msanii machachari sana wa nyimbo za kwaya JOSEF NYUKI nae alikuja na kufanya nae kazi na wakatoa nyimbo yake ya TEGEMEO LANGU, na tena akafanya kazi na BAHATI BUKUKU na kumtengenezea mwimbo wake wa NIMESAMEHEWA DHAMBI SIO MAJARIBU…kisha akaja NESTA SANGA wakafanya UWAHONGERE,na hata ENOCK nae pia walifanya nae kazi katika mwimbo wa ZUNGUKA ZUNGUKA . Hivi sasa Kameta anamializia kazi ya msanii mwingine aitwae PIUS BUTOKE ambayo nayo anaamini itakua hit sana.  
MTAMBONI
                      Mwisho wa mazungumzo yake alisema   “natamani sana kufanya kazi na wasanii wa Mbeya,maana najua na kuamini kuna talent nying sana ziko Mbeya,nikifananisha na watu ninaofanya nao kazi,watoto wa Mbeya wako juu sana,sijui tatizo linakua nini,lakini kama wakitaka msaada toka kwangu nawakaribisha sana tuje tufanye nao kazi”alimalizia KAMETA.





No comments:

Post a Comment