Thursday, 24 October 2013

YANGA YAIFUNGA RHINO 3-0

                    Wakicheza kwa umakini,  timu ya Yanga ya Dar es salaam imefanikiwa kuwafunga Rhino Rangers ya Tabora kwa magoli 3-0,  goli moja likifungwa katika  kipindi cha kwanza na mawili kipindi cha pili katika mchezo ambao Yanga waliutawala kwa muda mwingi.
JUMA BADUL  AKIMUACHA VICTOR HANGAYA WA RHINO

    Mshambuliaji wa Yanga Mrisho Ngasa aliwasumbua sana walinzi wa pembeni wa Rhino kwani hawakua na njia nzuri ya kumzuia na kumfanya apige pasi na krosi nyingi kuelekea langoni mwa Rhino.  Na Simon Msuva alianza mchezo huo vizuri na kwa umakini mkubwa lakini kadri muda ulivyozidi kwenda alipoteza umakini na kufanya maamuzi mengi ambayo hayakua na uhakika,na akawa anajiangusha ili  apate faulo matokeo yake akapewa kadi ya njano. Alikuja kutolewa katika dakika ya 59.
            Yanga walibadili kikosi chao tofauti na kilichozoeleka na ambacho kilicheza na Simba katika sare ya 3-3,  walimuweka Juma Abdul kama beki wa kulia badala ya Mbuyu Twite aliyecheza beki wa kati,  na Zahir Rajab katika kiungo wa chini nafasi ya Atumani Iddi na mbele akaingia Simon Msuva  ambae alicheza pembeni na  katikati akasimama Hamisi Kiiza na Mrisho Ngasa,hivyo Athumani Iddi,Didier Kavumbagu na Nadir haroub hawakupangwa kabisa,na golini alikuwepo Deogratius Munishi badala ya Ally Mustafa.
HAMISI KIIZA AKISHANGILIA GOLI
             Goli la kwanza la Yanga lilipatikana baada ya Simon Msuva kupokea mpira toka kwa Zahir na akakimbia pembeni akimuacha kirahisi beki wa kushoto wa Rhino Hussein Abdallah na kupiga krosi iliyompita Ladislaus Mbogo na kumkuta Kiiza aliyeupeleka wavuni,ilikua ni dakika ya 12. Waliendelea kutawala na kuwapoteza kabisa viungo wa Rhino Stanslaus Mwakitosi,Imani Ndeli na Nurdin Bakari ambao muda mwingi walikua wakiutafuta mpira bila mafanikio.
               Yanga walifanikiwa kupata bao la pili katika dakika ya 72 lililofungwa na kiungo wao Frank Domayo aliyemalizia kazi nzuri ya Mrisho Ngasa aliyempita kwa umaridadi beki wa kushoto WA Rhino na kutoa pasi nzuri kwa Domayo aliyemalizia kirahisi.Rhino hawku na mipango ya kutafuta goli kwani hata golikipa wa Yanga Meogratius Munishi  hakuokoa hata hatari moja,muda wote wa mchezo alikua kama mtazamaji.
MBUYU TWITE AKIMDHIBITI IMANI NDELI

                   Goli la tatu lilifungwa tena na Hamisi Kiiza na kumfanya afkishe magoli saba katika ligi hii,lilipatikana baada ya mpira ulioppigwa na Ngasa kumshinda Nurdin Bakari aliyeteleza na kuanguka na mpira kumfikia Kiiza aliyeupeleka pembeni mwa goli la Rhino na kuandika goli la tatu.Kwa ujumla Yanga walicheza vizuri sana katika mchezo huo na kutengeneza nafasi nyingi za kufunga tofauti na Rhino ambao walikua kama hawajajitayarisha kwa ajili ya mchezo huo.
HAMISI KIIZA,DOMAYO,NIZAR NA NGASA 

            VIKOSI;
  YANGA-Deogratius Munishi,Juma Abdul,David Luhende,Mbuyu Twite,Kelvin Yondani,Zahir Rajab,Simon Msuva,Frank Domayo,Hamisi Kiiza,Mrisho Ngasa,na  Haruna Niyonzima.
   RHINO- Mahmoud Othman,Ally Mwanyiro,Hussein Abdallah,Julius Masonga,Ladislaus Mbogo,Stanslaus  Mwakitosi,Shija Mongo,Imani Ndeli,Victor Hangaya,Saad Kipanga na Nurdin Bakari.


                     

No comments:

Post a Comment