Monday, 21 October 2013






Simba
Ilivyo chomoa
kwa
yanga
      NA ABDUL SUDI.
KIKOSI CHA SIMBA

                   Wakati wa mapumziko,kila shabiki wa mpira Tanzania,iwe anatazama akiwa uwanjani au katika televisheni,au awe anasikiliza katika radio aliamini kabisa Yanga wameshashinda mchezo huo,kilichokua kikisubiriwa ni idadi ya magoli yatakayoongezeka kipindi cha pili.kwani pamoja na kuongoza kwa magoli matatu walikuwa wameutawala mchezo katika idara zote,katikati Athumani Iddi,Frank Domayo na Haruna Niyonzima walikua wamepashika vilivyo.Mrisho Ngasa na Didier Kavumbagu walikua wanasumbua sana,na Hamisi Kiiza alikua akirudi kuwasaidia viungo na kuipeleka mipira mbele na kwa kasi waliyoku nayo Yanga,mchezo ulionekana tayari umekwisha.
KIKOSI CHA YANGA
                                                                                  
             Lakini sio kwa Kibaden na msaidizi wake Jamhuri Kihwelo,wao walikua na imani kua mambo yanaweza kubadilika,walitulia wakatazama nini tatizo,wakaona wametawaliwa katikati wakaamua kufanya mabadiliko yaliokua na manufaa makubwa katika mchezo huo,wakamtoa Chanongo ambae hakucheza katika kile kiwango alichozoeleka,wakamtoa na Humud ambae kwa vile alichezeshwa nafasi ambayo hakuizoea ya kiungo wa mbele, ilikua inamuwia ngumu sana kugawa mipira,alikua anakaba vizuri lakini anapotoa pasi alikua mara nyingi anawapasia maadui hivyo kufanya Jonas Mkude aliyecheza kiungo wa chini awe na kazi ngumu sana ya kuitafuta mipira iliyoharibika.
     Wakawaingiza watoto Wiliam Lucian,na Said Ndemla ambao kwa kiasi kikubwa ndio waliobadili sura ya mchezo.walisaidiana kukaba na kugawa mipira vizuri sana na kumfanya Mkude awe na sehemu kubwa sana ya kucheza katikati,na kutokana na kuchoka kwa Athumani Iddi Simba walitawala mno kiungo katika kipindi cha pili.na wakatengenza nafasi nyingi za kufunga na wakafanikiwa kuzitumia tatu kati ya hizo.
OWINO(KUSHOTO JEZI NYEKUNDU)AKIFUNGA GOLI LA PILI
Yanga walianza mchezo huo kwa nguvu sana kwa kupiga pasi nyingi na kuwachanganya Simba.na  kufanikiwa kupata bao la kwanza katika dakika ya 14 baada ya kazi nzuri sana iliyofanywa na Didier Kavumbagu kuwazidi nguvu na ujanja mabeki wawili wa Simba ambao walimfuata kwa pamoja na kumuacha Kiiza pembeni,hivyo Kavumbagu alivyogombea nao mpira alifanikiwa kuusogeza hadi kwa Kiiza ambae alipiga krosi na kipa wa Simba alitaka kutoka akasita na ndipo mpira ukamkuta Mrisho Ngasa aliyepiga mini volley na mpira kupita pembeni juu ya lango la Simba na kuandika bao la kwanza.

       Hawakuachia hapo kwani waliendelea kushambulia na kufanikiwa kupata bao la pili kupitia kwa Hamisi Kiiza baada ya mabeki wa Simba kushindwa kuuzuia mpira uliorushwa na Mbuyu Twite na kumkuta Kiiza aliyeusukumiza wavuni.Simba wakapoteana na Yanga wakazidi kucheza kwa uhakika,Chanongo akawa anashindwa kumsaidia Haruna Shamte ambae muda mwingi alijikuta anaingia katikati kwenda kuwasaidia mabeki na viungo hivyo pembeni Ngasa akawa huru sana,Athumani Iddi akawa anapiga pasi pembe zote na Niyonzima akasogea sana katikati na kuwafanya viungo wa Simba kushindwa kuhimili nguvu kubwa ya Yanga.
MOMBEKI AKIWAHI KUANZISHA MPIRA BAADA YA GOLI LA PILI LILILOFUNGWA NA OWINO
                Goli la tatu la Yanga lilipatikana kutokana na uzembe uliofanywa na Ramadhan Singano  baada ya kupata pasi kutoka kwa Cholo akataka kupiga chenga lakini hakuweza hivyo akataka kuurudisha kwa Cholo kwa kisigino na Yanga wakaunasa na wakapiga mpira mrefu uliomkuta Kavumbagu aliyemzidi mbio Cholo na kutoa pasi kwa Kiiza aliyeukwamisha wavuni na kuandika goli la tatu.
               Wachezaji wa Yanga wakaona wamemaliza mchezo wakawa wanacheza kwa mbwembwe  na hasa Mrisho Ngasa na Nadir Haroub,wakawa  wanaucezea mpira wanavyotaka,hawakujua kua wanawapa Simba nafuu kwani tayari walikua wamepoteana.
Hadi mapumziko Yanga wakawa wanaongoza kwa magoli matatu kwa bila.
                Kipindi cha pili Simba walifanya mabadiliko baada ya kuwatoa Humud na Chanongo n nafasi zao kuchukuliwa na Said Ndemla na Wiliam Lucien ambao wakaubadilisha mchezo kwa kila hali.Wakamsaidia Mkude kukaba katikati na kuvuruga mipango ya Yanga,na kwa vile Athumani Iddi alikua tayari kachoka akawa anacheza nyuma sana hivyo kuwafanya viungo wa Simba kummeza Domayo,na Niyonzima akawa hapati tena mipira toka katikati.wakafanikiwa kupata bao la kwanza kupitia kwa Betram Mombeki aliyepata pasi nzuri toka kwa Hamis Tambwe aliyekimbia na mpira hadi pembeni mwa lango la Yanga  na kupiga pasi iliyomkuta Mombeki na akaupiga kiufundi na kuandika bao la kwanza.
KELVIN YONDANI AKIWA HAAMINI
                   Simba wakazidi kuchangamka na Yanga wakapoteana,kwa vile Niyonzima alikua akiingia sana katikati,Nassor  Cholo akawa huru sana upande wa kulia na kumfanya muda mwingi kucheza kama mshambuliaji,na alisababisha matatizo mengi sana kwa mabeki wa Yanga, kwani magoli yote yalitokea upande wa kulia.
     Goli la pili lilitokana na kona upande huo huo wa kulia na Ramadhani Singano alipopiga hiyo kona ilimkuta Josef Owino aliyepiga kichwa na kuandika goli la pili.Yanga wakaamua kumtoa Kiiza na nafasi yake kuchukuliwa na Simon Msuva,mabadiliko yaliyowamaliza kabisa nguvu Yanga kwani hawakuwa tena na mipango ya kushambulia.Msuva na Ngasa wote wakawa wanacheza upande wa kulia na Niyonzima akawa kaingia sana katikati hivyo pembeni upande mmoja  kwa Yanga hakukua tena na mtu,Simba wakawa wamekamata kabisa katikati.
    Ngasa alipata nafasi ya kumaliza mchezo baada ya kuwatoka mabeki wawili wa Simba lakini uhodari wa kipa wa Simba Abel Dhaira ulimkosesha goli kwani aliokoa ikawa kona ambayo haikuzaa matunda.
GILBERT KAZE

                   Simba walipata bao lao la tatu kupitia kwa beki  wake wa kati Gilbert  Kaze baada ya faulo iliyotokea upande ule ule wa kulia ikapigwa na Nassor Cholo na kumkuta Kaze akiwa hana mtu wa kumkaba kwani mabeki wawili wa Yanga walikua wamemkaba Mombeki na hivyo Kaze akapiga kichwa na kuandika bao la tatu.

WACHEZAJI WA YANGA WAKILAUMIANA BAADA YA KUINGIA GOLI LA TATU
                              Simba wakapata sare ambayo wala hawakuitarajia.kwa kiasi kikubwa yanga walitakiwa kushinda hii mechi lakini hawakua makini katika kuulinda ushindi wao na kudhania mechi tayari imekwisha.

No comments:

Post a Comment