Saturday, 16 November 2013

      Alex seth
Messi wa
 mbeya city
IMEANDIKWA NA ABDUL SUDI,PICHA KWA HISANI YA ALEX SETH

       Anapiga miguu yote miwili, jambo ambalo ni nadra sana kwa wachezaji wengi,  ana uwezo wa kufunga na pia ni mzuri sana  wa kupiga pasi za mwisho.  Huyo ni Alex Seth au maarufu sana kwa mashabiki wa soka kama Messi wa Mbeya City.
KABLA YA KUPAMBANA NA YANGA
           Ingawa  ana umri mdogo wa miaka 19, lakini si muoga kwa mabeki hata wale wanaosifika kwa kucheza faulo, anavyozidi kufanyiwa faulo,  inakua kama unampa hamu zaidi ya  kutaka kupita kwa lazima, atakupiga chenga, atakutoka kwa kasi na pia anatoa krosi nyingi zenye akili.

ALEX (WA PILI KUSTOKA KUSHOTO MBELE) AKIWA NA KIKOSI CHA CITY 
    Alizaliwa mkoani Ruvuma na kupata elimu yake hapo hapo Ruvuma katika shule ya sekondari Msamala, na alikua ni mchezaji wa kutumainiwa wa timu ya shule,na hata katika timu ya Kambarage kids kisha MajiMaji ikiwa daraja la kwanza. 
WAKATI WA MCHEZO NA JKT OLJORO
          Alipomaliza kidato cha nne kocha Juma Mwambusi aliamua kumchukua ili wasaidiane kuipandisha daraja timu ya Mbeya City, jambo ambao walilitimiza na kufanikiwa kuingia katika ligi kuu.
      Na hata timu ilipopanda amefanikiwa kucheza mechi  kadhaa, ikiwemo mechi ya kwanza kwa Mbeya City kucheza ligi kuu ya Tanzani pale walipocheza na Kagera Sugar. Toka hapo ameweza kucheza michezo kumi kati ya kumi na tatu timu yake iliyocheza.
BAADA YA MECHI NA MGAMBO MKWAKWANI TANGA
     Akiizungumzia timu yake ya Mbeya City anasema kikubwa kinachowafanya wafanikiwe hadi kufikia hatua hii ni jinsi walivyo pamoja kwani mchezaji hata ambae hakucheza katika mchezo husika hua anashiriki kwa asilimia mia moja kuhakikisha anawapa hamasa wale wanoacheza, hakuna mazengwe kama wanayoyasikia kwa timu nyingine.
ALEX (WA KWANZA KUSHOTO)WAKATI WA MECHI NA SIMBA,UWANJA WA TAIFA
       Pia hakusita kuwasifia mashabiki wa timu hiyo kwani kila wanapocheza wanakua kama wana kitu cha ziada nje  kinachowasukuma wafanye vizuri .  “tazama mchezo  wetu na Azam, tulicheza ugenini lakini jinsi  mashabiki wetu walivyokua wengi ilikua kama tunacheza jijini Mbeya! Walikua ni zadi ya nusu ya uwanja, ukitazama wengi walikua wamesafiri kuja kutupa sapoti, hilo nalo linaongeza nguvu na kutufanya tupigane ili tusiwaangushe.”alisema.
MASHABIKI WA MBEYA CITY KABLA YA MECHI NA AZAM
     “Na  kitu kingine kinachotufanya  tuwe makini ni  ubora wa kocha wetu Juma Mwambusi, kwani  yupo karibu sana na sisi na habagui mchezaji, kama anakuweka benchi  anakuambia kabisa sababu ya kukuweka benchi hivyo unakua na amani na kujua nafasi yako bado ipo vile vile tatizo tu ni mipango ajili ya mechi husika,  ni mmoja kati ya makocha bora sana hapa nchini”alimalizia .
KOCHA JUMA MWAMBUSI

       Seth ambae ni bingwa wa kupiga chenga na kubadili muelekeo kila anapoona njia zimeziba, amesema ana matarajio ya kujifua sana wakati huu wa mapumziko ili awe mzuri zaidi katika duru la pili….hawakukosea kumwita jina la Messi….. 

No comments:

Post a Comment