Sunday, 17 November 2013

IVORY COAST YAINGIA KOMBE LA DUNIA

      Goli lililofungwa dakika za nyongeza na  Salomon Kalou lilitosha kuwapa nafasi  Ivory Coast kuungana na Nigeria kutinga katika kombe la dunia nchini Brazil 2014.

     Katika  mchezo wa kwanza Ivory Coast walitoka na ushindi wa magoli 3-1 katika mchezo uliochezwa jijini Abidjan Ivory Coast.
       Senegal walikua wa kwanza kupata bao baada ya mshambuliaji
 wa Ivory Coast Didier Drogba kumfanyia faulo mshambuliaji wa Senegal Sadio Mane na mwamuzi kuamuru ipigwe penati na Sow akaikwamisha wavuni na kuwafanya Senegal wawe mbele kwa goli moja.

          Senegal walihitaji goli moja ili iwe 2-0 na wapite kwani wangekua na faida ya goli la ugenini, na dakika 15 za mwisho walishinda golini mwa Ivory Coast na kufanya mashambulizi mengi ya nguvu lakini kipa Boubacar Bary alijitahidi kuokoa.

               Katika dakika za majeruhi Senegal walifanya shambulizi kali na kupata kona lakini Salif Sane akakosa goli la wazi na mpira ulivyorudi upande wao Yaya Toure alitoa pasi nzuri kwa Salomon Kalou aliyefunga na kuamsha shangwe nchini Ivory Coast.

          Mchezo huo ulichezwa jijini Casablanca Morocco badala ya nchini Senegal baada ya nchi hiyo kufungiwa kutumia viwanja vyake kutokana na vurugu.
      Ivory Coast imeungana na Nigeria na kua timu ya pili toka Africa kutinga katika kombe la dunia litakalofanyika nchini Brazil.

No comments:

Post a Comment