Wednesday, 13 November 2013

Manow tukuyu mbeya
      Manow  ni moja ya sehemu tulivu na yenye uoto mzuri wa asili na mazingira yake ni mazuri mno nay a kupendeza. Ipo katika wilaya ya Rungwe, karibu kabisa na mlima Kyejo, mlima ambao una volcano
iliyokufa. Manow pia iko katika sehemu inayopatikana gesi ya ukaa (carbon dioxide) ambayo inatumika katika ukanda wote wa Afrika mashariki na kusini.
MANOW
      Manow ipo kilomita 47 toka Tukuyu mjini na ukitokea Mbeya mjini ni kilomita 120. Ni sehemu ambayo inapendeza sana na mandhari yake inakufanya upende kuendelea kukaa.
MLIMA KYEJO
            Kuna baridi muda wote wa mwaka, ni nadra sana kwa miezi mingine hata kuliona jua, Mvua inayesha zaidi ya nusu ya mwaka, hivyo kufanya wakulima walime mwaka mzima , na uzuri wa Manow,hakuna zao linalogoma kuota labda yanayoota pwani tu ila kila kitu kinakubali. Na kwa vile ardhi yake ina rutuba sana mazao kama karoti, viazi,ndizi,matunda ya aina zote, mahindi, maharage ,maparachichi (makatapera) na kila aina ya mazao yanaota vizuri sana.
LWANGWA
        Kinachofurahisha zaidi, hakuna magonjwa ya kuambukiza Manow,  magonjwa kama Malaria na Typhoid hayapo kabisa  na ukiona mtu anaumwa ugonjwa huo jua amekuja nao toka sehemu nyingine. Pia maji yake ni safi  na salama haina haja ya kuyachemsha, vyanzo vya maji ni salama na  visafi hivyo hakuna hatari kama sehemu nyingine za Tanzani.
MBIGIRI
         Kuna shule nzuri ya Manow ambayo ipo kidato cha kwanza  hadi kidato cha sita,  ni shule ya mchanganyiko, wavulana na wasichana , na ni nzuri kutokana na majengo na pia ni nzuri kwa ubora wa elimu wanayoitoa,shule hiyo inamilikiwa na kanisa la KKKT dayosisi ya konde, na hilo linazidisha umakini wa elimu inayotolewa na kupokelewa hapo shuleni.
SHULE YA MANOW

   Watu wengi toka mkoa wa Mbeya na sehemu nyingine za Tanzania na nje ya Tanzania  wamesoma katika shule hii ya Manow.
MANOW SEKONDARI

       Mandhari ya Manow ni ya kupendeza sana, Asubuhi kunakua na  ukungu ambao unazidi kupendezesha na pia, Mlima Kyejo ni moja ya sehemu zinazovutia sana kuzitama, Manow ni sehemu nzuri, safi na inavutia sana, ni moja ya sehemu zinazovutia sana Tanzania.

No comments:

Post a Comment