Saturday, 30 November 2013

       ARSENAL BALAA
      yaifunga Cardiff 3-0

       Aaron Ramsey alifunga magoli mawili dhidi ya timu yake ya zamani ya Cardiff katika ushindi mnono wa magoli 3-0 walioupata Arsenal.

        Ramsey ambae kwa sasa yupo katika iwango kizuri alifunga goli la kwanza kwa kichwa katika dakika ya 29 baada ya kupokea krosi toka kwa Ozil na kupiga kichwa na mpira kumshinda kipa aliyekua kasogea mbele.

      Goli hilo lilishangiliwa na mashabiki wa timu zote mbili, wa Arsenal  na wa Cardiff timu ambayo Ramsey aliihama mwaka 2008 na kujiunga na  Arsenal.

           Kabla ya hapo, Olivier Giroud alikosa goli la wazi pale alipobaki na kipa wa Cardiff baada ya kupokea pasi nzuri sana ya Ozil lakini akasita kuupiga mpira akidhani ameotea na hadi alipoamua kupiga tayari akawa amechelewa. 
            Cardiff walijitahidi kutafuta bao la kusawazisha na walikosa nafasi mbili nzuri moja akiikosa Campbell alipopiga kichwa na kipa wa Arsenal akautoa nje na nyingine nzuri ni kichwa kilichopigwa na Ben Turner lakini mpira ukatoka juu kidogo ya goli.

           
  Arsenal walipata bao la pili dakika ya 86  kupitia kwa Matheu Flamini aliyepiga shuti kali akiwa karibu na goli baada ya kupata pasi toka kwa Carzola.

         Ramsey aliongeza bao la tatu katika dakika za majeruhi baada ya kuupata mpira uliookolewa kutokana na shambulizi lililofanywa na Cardiff.

   

          

No comments:

Post a Comment