Saturday, 7 December 2013

Man u yachapwa

Manchester United imefungwa kwa mara ya pili mfululizo katka uwanja wa nyumbani wa Old Traford, kwa goli lililofungwa na Yohane Cabaye katika dakika ya 61, na kuifanya Newcastle United  kuishinda Manchester United kwa mara ya kwanza katika uwanja huo toka mwaka 1972.

     United hawakucheza vizuri katika mchezo huo, kwani hakukua na mpango mizuri ya kutafuta goli na haikushangaza hadi kipindi cha kwanza kinakwisha walikua wamefanya shambulizi moja tu langoni mwa Newcatle.

       Kipindi cha pili angalau kidogo walishambulia pale kichwa kilichopigwa na Patrice Evra kiliokolewa na Anita katika mwamba wa goli,  na pia Robin Van Persie aliweza kutumbukiza mpira golini lakini ikawa ni off side.

    Newcastle walipata goli lao la ushindi kupitia kwa Yohan Cabaye aliyepokea krosi  toka kwa Mousa Sissoko ambae alifanya kazi nzuri ya kumpita Patrice Evra.

       Kwa matokeo hayo Man imepoteza point 13 hadi sasa katika uwanja wake wa nyumbani, hali iliyowafanya mashabiki wengi watoke uwanjani kabla hata mchezo haujaisha.


         

No comments:

Post a Comment