Sunday, 17 November 2013

Cameroon ndani kombe la dunia

Cameroon wamepata ushindi mnono wa mabao 4-1 dhidi ya Tunisia na kujihakikishia nafasi ya kushiriki kombe la dunia litakalofanyika nchini Brazil 2014.
JEAN MAKOUN

          Walipata goli la kwanza mapema kabisa katika dakika ya 3  ya mchezo lililofungwa na Piere Webo baada ya kumpokonya mpira  beki wa Tunisia Karim Haggui na kupiga shuti kal la chini la kushoto lililompita kipa wa Tunisia na kuingia golini.
MAKOUN AKIMTOKA MLINZI WA TUNISIA
       Moukandjo aliipatia Cameroon bao la pili katika dakika ya 31 baada ya kuwapita mabeki watatu wa Tunisia na kupiga mpira ulioingia pembeni na kuhesabu goli la pili.

      Akaichi aliipatia timu yake ya Tunisia bao baada ya kuunganisha kwa mguu wa kushoto baada ya kumzidi mbio mlinzi wa Cameroon Aurelion Chedjou.
     Makoun aliipatia Cameroon bao la tatu kwa kichwa baada ya kuunganisha kona iliyopigwa na Assou  Ekoto .na baadae akafunga goli la nne na la mwisho na kuwahakikishia Cameroon nafasi ya kucheza katika kombe la dunia.


  Cameroon wamekua nchi ya tatu kufanikiwa wakizifuata timu za Nigeria na Ivory Coast zilizokwishapita.

No comments:

Post a Comment