Monday, 18 November 2013

UHURU ARUDI SIMBA

Uhuru Selemani amerudi katika timu ya Simba baada ya kuitumikia timu ya Coastal Union kwa mkopo.

       Ni mmoja kati ya wachezaji wenye kipaji cha hali ya juu sana cha soka, anaeweza kucheza kama kiungo wa pembeni, na pia ana uwezo mkubwa wa kucheza kama mshambuliaji,

     Sifa yake kubwa ni uwezo alio nao wa kupiga chenga za kwenda mbele, na kupiga mashuti kwa miguu yote miwili, pia ana uwezo mkubwa wa kupiga shuti huku anakimbia, hivyo mara nyingi anawapa taabu sana mabeki wanaojaribu kumzuia.

              Akiongelea kuhusu kurudi kwake katika timu ya Simba Uhuru alisema  “zimebaki hatua chache sana kwangu mimi kurudi Simba,na mimi binafsi sina kipingamizi chochote, kwani pale ni nyumbani na napata faraja kuona bado nina uwezo wa kuitumikia timu yangu ya Simba,hivyo nipo tayari kuitumikia Simba”


    Hongera Uhuru  tunasubiri kuona vitu vyako adimu.

No comments:

Post a Comment