Sunday, 24 November 2013

Cardiff sare na man utd

Wayne Rooney  aliifungia Manchester United goli la kuongoza , lakini mchezaji wa zamani wa Manchester United  Frazer Campbell akaisawazishia Cardiff .

           Baadae Rooney akapiga kona iliyomkuta Patrice Evra aliyepiga kichwa na kufunga goli la pili, Cardiff wakasawazisha tena kupitia kwa mchezaji aliyeingia kipindi cha pili, Kim aliyefunga kwa kichwa sekunde chache kabla ya mchezo kumalizika na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa magoli 2-2.

         Rooney alikua na bahati ya kuendelea na mchezo huo kwani alimfanyia faulo mbaya mchezaj wa Cardiff Mutch lakini akapewa kadi ya njano na kutoa ahueni kwa mashabiki wa United.

       Campbell angeweza kuongeza goli pale mpira aliopiga ulipogonga mwamba wa goli na kurudi uwanjani.
      Katika dakika za mwisho United walipoteza nafasi kadhaa za kuweza kushinda mchezo huo, mbili alipoteza Danny Welbeck baada ya kubaki na golikipa na kushindwa kufunga, na moja aliipoteza Wayne Rooney bada ya kupiga kisigino ili kumpa pasi Welbeck badala ya kufunga yeye mwenyewe.

         United hawakkucheza vizuri katika kiungo na hvyo kumfanya kocha David Moyes awe na kazi kubwa ya kufanya maana hata mchezaji Maloune Fellaini bado hajatoa msaada mkubwa kama ilivyotegemewa.

         

No comments:

Post a Comment