Tuesday, 19 November 2013

Deus kaseke
Engine ya mbeya city

     Ana kasi ya ajabu, anazunguuka uwanja mzima , anapiga chenga  na kutafuta nafasi  kila muda anaokua hana mpira, Si ajabu hadi leo mashabiki wa Simba bado wanamzungumzia, kwani aliwasumbua viungo na walinzi wa timu hiyo kupita maelezo
.
      Alizaliwa Nzovwe jijini Mbeya na kuanza kucheza soka toka akiwa shuleni, na hata alipofika sekondari katika shule ya Kalobe alikua ni mchezaji wa kutumainiwa wa timu ya shule.
DEUS KASEKE(pich na deus kaseke)

      Wakati akisoma alikua pia akiichezea timu ya African Boys ya Nzovwe, na hapo ndipo kipaji chake kilipozidi kuimarika kwani alikuta vijana weng ambao pia walikua na kipaji cha soka na kuifanya timu hiyo kua moja kati ya timu nzuri jijiniMbeya.

      Alipomaliza sekondari akachukuliwa na timu ya Polisi Iringa (ambayo sasa ni Lipuli)na akacheza kwa muda kisha baadae ndipo akafuatwa na kocha Juma Mwambusi na kujiunga na timu ya Mbeya City.
DEUS KASEKE

         Pamoja na ushindani alioukuta katika timu hiyo, hua anapata nafasi mara kwa mara,  na mara nyingi amechezeshwa kama kiungo mshambuliaji anaetokea pembeni, iwe upande wa kushoto au kulia, ingawa hua anazunguuka uwanja mzima.
         Amekua ni kama injini ya timu kwani magoli mengi hua yanatokea upande wake, iwe kwa kupiga pasi ya mwisho au hata kuanzisha move ya goli.Ni mzuri sana hasa anapobakia na beki mmoja au wawili, hua anawamaliza kirahisi hadi mtazamaji anaona kama wanafanya makusidi kupitwa.
DEUS KASEKE AKIWATOKA AGREY MORIS NA HUMPHREY MIENO WA AZAM
       Katika sare ya magoli 2-2 na Simba alimsumbua sana mlinzi wa kushoto wa Simba Issa Rashid baba ubaya kiasi mchezo ulipokwisha aliyekua kocha wa Simba alimlaumu mno huyo beki kua ndie aliyesababisha hiyo sare,kwani alikua anapitwa kirahisi na Deus.
DEUS AKIMUACHA WAZIR SALUM WA AZAM
         Hata katika mchezo  wa mwisho wa raundi ya kwanza dhidi ya Azam,aliwafanya mabeki Erasto Nyoni, Said Morad,Waziri Salum na Agrey Moris washindwe kabisa kumzuia,kwani alikua akiwapita anavyotaka, hata goli la kwanza lililofungwa na Mwegane Yeya alipiga krosi mbele ya Nyoni huku wakiwa wamesimama na wanatazamana.
DEUS AKIINGIA NDANI YA BOX HUKU AKITAZAMWA NA AGREY NA SAID MORAD

     Deuse Kaseke ni mmoja kati ya wachezaji ambao wana nafasi kubwa sana ya kufanya mabadiliko ya soka nchini Tanzania, haitakua ajabu kusikia kapata timu na kwenda kucheza nje ya nchi, kwani kiwango chake ni kikubwa sana kwa ligi ya Tanzania.

No comments:

Post a Comment