Wednesday, 20 November 2013

RONALDO AIPELEKA URENO BRAZIL

               Ronaldo akiwa katika kiwango chake bora kabisa amefanikiwa   kuisaidia nchi yake kuingia katika fainali za kombe la dunia zitakazofanyika nchini Brazil mwaka 2014.

       Katika mchezo wa kwanza Ureno walishinda kwa goli moja lililofungwa na Ronaldo,hivyo walikwenda Sweden wakiwa na faida ya hilo goli.
        Kipindi cha kwanza hakukua na goli lolote na kasi ilikua ni ndogo lakini mambo yalikuja badilika katika kipind cha pili,Ronaldo alikua wa kwanza kuipatia timu yake goli la kwanza katika dakika ya 50.

          Ibrahimovic  alisawazisha kwa kichwa kufatia kona iliyopigwa na Kim Killstrom na kurudisha matumaini ya kuendelea.

         Ibrahimovic alifunga tena goli la pili baada ya
kupiga faulo na mpira kwenda moja kwa moja golini, na kuzidisha matumaini ya kuweza kuwatoa Ureno.  
          Lakini furaha ya wasweden ilikazimwa tena na Ronaldo aliyefunga goli la pili baada ya kupokea mpira toka kwa Almeida na kupiga shuti lilitinga wavuni.

         Hakuishia hapo kwani alifunga goli la tatu baada ya kumpiga chenga kipa wa Sweden na kisha kufunga goli la tatu lililowapeleka Ureno hadi katka fainali za kombe la dunia.hadi mchezo unakwisha Ureno 3 na Sweden 2.


        Kwa ujumla ilikua ni kama vta ya Ronaldo na Ibrahimovic,kwani macho yaw au wote yalikua yakiwatazama wao, na kwa mchezo wote wameonyesha mchezo wa hali ya juu sana na kufunga magoli muhimu, ingawa Ronaldo ndio anaondoka na ushindi maana tmu yake imefanikiwa kushinda.

No comments:

Post a Comment