Everton yaibana liverpool
Timu ya Everton imeibana
Liverpool kwa kutoka sare ya mabao 3-3 katika mchezo mgumu na wa kuvutia
uliofanyika katika uwanja wa Goodison Park.
Huu ni mchezo uliotoa magoli mengi katika mchezo uliozikutanisha timu hizo toka mwaka 1935.
Huu ni mchezo uliotoa magoli mengi katika mchezo uliozikutanisha timu hizo toka mwaka 1935.
Iliwachukua dakika tano kwa Liverpool
kupata bao la kwanza
lililofungwa na Coutinho akiunganisha kona iliyopigwa na Gerrard.Goli hilo lilichangiwa sana na uzembe wa mabeki kushindwa kujipanga vizuri.
lililofungwa na Coutinho akiunganisha kona iliyopigwa na Gerrard.Goli hilo lilichangiwa sana na uzembe wa mabeki kushindwa kujipanga vizuri.
Everton walisawazisha dakika tatu baadae
kupitia kwa Mirallas baaada ya Martin Skrtel
kushindwa kuzuia faulo iliyopigwa na Leighton Baines.
Luis Suarez aliongeza bao la pili baada ya kupiga faulo ya
chinichini na kumpita kipa wa Everton Tim
Howard.Faulo hiyo ilipatikana baada ya Gareth Barry kumfanyia madhambi Suarez.
Suarez baadae alifanyiwa faulo mbaya
na Mirallas lakini mwamuzi akampa kadi ya njano badala ya nyekundu kama wengi
walivyofikiria.
Katika mchezo uliozikutanisha hizo timu
msimu uliopita, Mirallas nae alifanyiwa faulo mbaya na Suarez na ilionekana kama
vile analipiza kisasi.
Everton walisawazisha kupitia kwa
Lukaku baada ya kupokea mpira toka kwa Mirallas ambae aliwasumbua sana mabeki
wa Liverpool. Kabla ya goli hilo, kipa wa Liverpool Mignolet aliweza kumzuia mara tatu mshambuliaji huyo hatari wa Everton.
Baadae Lukaku akafunga goli la tatu kwa kichwa akiunganisha kona iliyopigwa na Mirallas, ambae alicheza vizuri sana katika mchezo huo-ukiondoa faulo aliyomfanyia Suarez.
Lakini Liverpool hawakukata tamaa na wakafanikiwa kusawazisha
kupitia kwa Sturridge, aliyeingia mwishoni na ambae hakuanza kutokana na kutoka kupona majeraha aliyoyapata katika timu ya taifa, na kuufanya mchezo huo kumalizika kwa magoli 3-3









No comments:
Post a Comment