Juma mwambusi
Kocha aliyeleta mabadiliko ya soka Tanzania
Sasa hivi kila kona ya Tanzania
kinachozungumzwa sana kwa mashabiki wa soka ni juu ya timu ya Mbeya City.
Na cha kufurahisha kila mmoja
anaongelea jinsi wanavyotandaza soka maridadi na kuzipa shida timu zote ilizokutana nao.
anaongelea jinsi wanavyotandaza soka maridadi na kuzipa shida timu zote ilizokutana nao.
Walipoanza ligi ilionekana kama ni timu ya kawaida kama nyingine ilizopanda nazo
daraja, Ashanti na Rhino, lakini kila
ligi inavyoendelea ndivyo ubora wa Mbeya
City unazidi kuonekana,kwani katika
michezo kumi na tatu iliyocheza hajafungwa hata mara moja, na imeweza kumaliza
mzunguko wa kwanza ikishika nafasi ya tatu, wakipishana kwa magoli tu na timu
ya Azam iliyo nafasi ya pili.
Mafanikio ya timu hiyo yanatokana hasa
na umahiri wa kocha anaefundisha timu hiyo, Juma Mwambusi, ambae amefanya kazi inayoonekana na
kila mpenda soka wa Tanzania.
Akiongelea mafanikio ya timu hiyo kocha
Mwambusi amesema “Tulichofanya kwanza ni
kutafuta vipaji vya hapa hapa nyumbani,na kwa vile kuna mashindano mengi
yanayofanyika jijini Mbeya ilikua ni rahisi kuwafatilia walipokua wakicheza
mara kwa mara,hivyo hadi kufikia kumsajili unajua kabisa ana uwezo gani na
anacheza vizuri sehemu gani, Pili tulianza matayarisho mapema na kuwafanya
wachezaji wazoeane sana kabla hata ligi haijaanza, na hilo limetusaidia, kwani
kila mchezaji akipata nafasi anacheza kwa kiwango kile kile ambacho wengine
wanacheza.
![]() |
| KIKOSI CHA MBEYA CITY |
Na jambo la tatu ambalo ni kubwa
zaidi, nilisisitiza kusajli wachezaji wenye nidhamu,ambao bado wana kiu ya
mafanikio na inakua rahisi hata kuwafundisha na kufata maelekezo.Ndio maana
unakuta timu yangu wachezaji wana nidhamu na wanajituma toka mwanzo hadi
mwisho.”
Ingawa hakusita kusifia uongozi
wa timu hiyo na mashabiki wake. “Viongozi
wa timu yetu wanafanya kazi kubwa sana kujaribu kutimiza kila tunachohitaji na
wanatusikiliza kila tunapokua na matatizo,lakini pa mashabiki wa timu hii ni
mfano wa kuigwa,nawashukuru sana wanavyojitolea,wanasafiri kila mahali
tunapokwenda kucheza na wanashangilia mwanzo had mwisho,hata tukianza kufungwa
bado wanaendelea kushangilia kwa nguvu ile ile,wanafanya kazi kubwa sana,sisi
kama wachezaji tuna deni kubwa sana la kuwalipa hao mashabiki na kikubwa ni
kujituma kwa nguvu na kujitolea ili tupate ushindi”
| MASHABIKI WA MBEYA CITY WAKISHANGILIA KABLA YA MECHI NA AZAM |
Akiongelea kuhusu mchezo wa
mwisho walocheza na timu ya Azam alsema “kuna mapungufu ya maamuzi lakini hilo
si la kusema sana kila mtu aliona ila
kikubwa kilichotokea ni kwa vile vijana wangu hawakuzoea kucheza katika
nyasi bandia,tulifanya mazoezi kidogo
uwanja wa Karume siku moja kabla ya mechi, lakini kwa siku moja huwezi
kuzoea,ndio maana utaona hata goli la tatu beki wetu aliteleza kutokana na
nyasi hizo.”
| MOJA YA MABASI YALIOLETA MASHABIKI WA MBEYA CITY KUCHEZA NA AZAM |
“Watu wengi hawakuamini kama
tutafika hapa tulipofika,wengi walijua ni nguvu ya soda, lakini sasa hivi kauli zao zimebadilika,ninajivuna
kwa vile nina kikosi kikubwa,wanaocheza ni 11 lakini wapo wengine nje zaidi ya
18 wana uwezo sawa sawa na hawa wanaocheza, ndio maana hata mabadiliko
nikifanya anaeingia anafanya vizuri kama aliyetoka,mfano mwanzoni alikua
akifunga magoli Mwegane Yeya,lakini alipokuja kucheza Peter Mapunda nae
akatufungia mfululizo magoli muhimu sana na sasa hivi hapa kafunga tena
Mwegane,kwa hiyo najivunia sana vijana wangu na kwa njia hii nadhani tutafika
sehemu nzuri ligi itakapofika ukingoni.”


No comments:
Post a Comment