Sunday, 10 November 2013

Sunderland yaifunga man city

Manchester City imepoteza mchezo wanne katika ligi kuu ya Uingereza, baada ya kufungwa goli 1-0 na tmu ya sunderland.
Goli pekee katika mchezo huo lilifungwa na Phil Bardsley katika kipindi cha kwanza baada ya kumtoka James Milner na kuukata ukaingia pembeni mwa goli.
PHIL BARDSLEY  AKIFUNGA GOLI LA USHINDI
      Baada ya kufungwa goli hilo Man city walilishambuli mfululizo lango la Sunderland, lakini kazi kubwa ilifanywa na walinzi na golikipa wao Vito Manone, walijipanga vizuri na kuhimili misukosuko yote iliyokua ikielekezwa langoni mwao.
PHIL BARDSLEY AKISHANGILIA
        Mlinzi wa Sunderland Wes Brown ambae alikua nje ya uwanja kwa miezi 22 kwa majeruhi alishirikiana vizuri na beki mwenzake walietoka nae Manchester United John O’shea  kuweza kuwazuia washambuliaji wenye uchu Sergio Aguero na Alvaro Negredo wasilete madhara.
WES BROWN AKIPAMBANA NA NEGREDO
         Dakika kumi za mwisho,Man City walizidisha mashambulizi na  Eden Dzeko allipiga shut lililopanguliwa kwa ngumi na kipa Vito.na baadae Aguero alipiga shuti  lililodakwa na kipa huyo.
SERGIO AGUERO

No comments:

Post a Comment