Thursday, 7 November 2013

  MASHABIKI WA MBEYA CITY WALIVYO  AMSHA AMSHA  DAR

Mamia ya mashabiki wa Mbeya City waliosafiri toka mbeya wameleta burudani kubwa uwanjani katika mchezo wa Azam na Mbeya City.
Licha ya kua walikua ugenini lakini yeyote aliyeona jinsi walivyojaa na kushangilia bila kuchoka angeamini walikua wanacheza uwanja wa nyumbani.
SHABIKI WA MBEYA CITY GWAKISA  NA NYUMA YAKE LORI LILILOLETA MASHABIKI WA KUKODIWA WA AZAM
       Pamoja na timu ya Azam kuleta mashabiki wa kukodi waliofika uwanjani kwa kutumia magari ya fuso,lakini walishindwa kuhimili amsha amsha ya mashabiki hao kutoka Mbeya.Kuanzia saa tano asubuhi walianza kufika kwa makundi na hata walipoambiwa tiketi zimekwisha walizidi kumiminika na kufanya uongozi wa soka kuuza tiketi za ziada tofati na makubaliano ya mwanzo.

SHABIKI WA AZAM ALIYEWATUKANA WATU WA CITY
      Kivutio kikubwa kilikua pale shabiki wa timu ya Azam ambae alikataa kutaja jina lake alipowafata na kuwatukana akitamba kwamba hawana uwezo wa kumfanya kitu,alishangaa alipojikuta amezungukwa na kundi kubwa la mashabiki wa Mbeya City kila mmoja akitaka kumpiga,alikua mpole na kuomba msamaha lakini baada ya kupata vibao kadhaa huku wenzake wakikimbia bila ya kumpa msaada.

AKIPATA KICHAPO
          Kichapo kilipomzidia alilia kwa sauti kubwa ndipo mashabiki wengine wa Mbeya City walipoamua kumsaidia na kumuondoa eneo hilo huku akilia kama mtoto.
WAKIMUONDOA BAADA YA KUOKOLEWA
           Kwa ujumla mashabiki hao wameshangilia muda mwingi kwa amani na furaha kubwa hata pale timu yao ilipokua nyuma walizidi kushangilia ili kuwapa moyo.
SHABIKI MAARUFU TOKA MWANJELWA MBEYA, GWAKISA AKIWA NJE YA UWANJA AKISUBIRI KUINGIA
      Mmoja kati ya hao mashabiki aliyejitaja kwa jina la Gwakisa toka mwanjelwa Mbeya alisema amekuja kushangilia timu yake kwa vile anajua ni wazuri hivyo anaona rah asana kuishangilia,alisema ana uhakika AZAM hawana uwezo wa kuifunga Mbeya City,na ukweli hawajawafunga.

    

No comments:

Post a Comment