MAN UNITED MBABE WA ARSENAL
Toka ajiunge na timu ya Manchester United akitokea timu ya Arsenal,Robin Van Persie amefanikiwa kuifunga timu yake ya zamani kila wanapokutana nayo, wamekutana mara tatu na kafunga mara tatu pia.
![]() |
| VAN PERSIE AKIFUNGA GOLI LA USHINDI |
Alifunga kwa kichwa katika dakika ya
27 kufuatia kona iliyopigwa na Wayne Rooney na kuipa timu yake ushindi muhimu katika
wakati mufaka.
Kwa matokeo hayo, Manchester
wamesogea hadi nafasi ya tano ya msimamo wa ligi kuu ya Uingereza, na kuwafanya
mashabiki wao kutulia.
![]() |
| VAN PERSIE AKISHANGILIA |
Katika dakika 15 za mwanzo mpira ulichezwa sana katikati ya uwanja na Manchester United walicheza kwa nguvu sana
kujaribu kuzuia na kushambulia kila wanapopata nafasi na kuwafanya Arsenal
washindwe kucheza mchezo waliozoea.
![]() |
| VAN PERSIE AKIZONGWA NA FLAMINI |
Manchester walipata goli lao katika
dakika ya 27 baada ya shambulizi kali lililofanywa na Wayne Rooney na Thomas
Vaemaelen akaupiga kichwa na kua kona iliyopigwa na mwenyewe Rooney na Van
Persie akapiga kichwa kilichoingia langoni mwa goli la Arsenal.
Kablaya mapumziko United walipata pigo
baada ya beki wake Nemanja Vidic kuumia na kutolewa baada ya kugongana na kipa
wake David De Gea wakati akiokoa mpira.
![]() |
| VIDIC AKITOKA BAADA YA KUUMIZWA |
Kipindi cha pili Arsenal walitulia na
wakapanga mashambulizi yao vizuri lakini alikua ni Wayne Rooney aliyekosa goli
la wazi pale mpira uliopigwa na Van persie ulimkuta Shinji Kagawa nae akampa
pasi Rooney aliyepiga kwa mguu wa kushoto na mpira ukatoka nje pembeni kidogo
ya goli la Arsenal.
Hadi mchezo unaisha United walitoka na
ushindi wa hilo goli moja.





No comments:
Post a Comment