Wednesday, 13 November 2013

NJIA 40 ZA KUISHI KWA FURAHA BILA MAJUTO

FURAHA NI KITU KIKUBWA SANA KATIKA MAISHA,FURAHIA MAISHA USIWE NA MANUNG’UNIKO WALA MAUDHI MOYONI…..HIZI NI NJIA 40 ZA KUKUSAIDIA KUISHI KWA FURAHA………
1.ELEWA NA KUKUBALI KWAMBA KUFANYA MAKOSA NI JAMBO LA KAWAIDA
(kufanya kosa ndio kujifunza)
2.AFYA YAKO IWE MUHIMU KWAKO
(jali afya yako,ukijisikia uko tofauti japo kidogo nenda katibiwe na wataalam,usinywe dawa kwa mazoea)
3.FATA MAAMUZI YAKO USIAMULIWE
(kua na msimamo wa unachoona ni kizuri,usikubali kuburuzwa)
4.JARIBU KUFANYA MAMBO YATAKAYOKUFURAHISHA,EPUKA YATAKAYOKUKERA
(epuka maudhi,kwani mwisho wake ni hasira na karaha)
5.KUA MTULIVU,USIHARAKISHE KUFANYA JAMBO LOLOTE
   (chunguza kila kitu kwa makini kabla hujaamua kukifanya)
6.KUA MDADISI,USIHOFU KUJARIBU JAMBO JIPYA
(usikubali kufanya kitu kwa kuelezwa tu kua ni kizuri,uliza unachoona kinakutia mashaka)
7.SOMA SOMA KILA WAKATI,UPANUE MAWAZO
(kila unaposoma kitu kipya.akili yako inazidi kutanuka,soma kila unapopata muda)
8.FURAHIA MAMBO NA WATU TOFAUTI
(jichanganye,usiwe kila mara mpweke)
9.JIWAZIE KWANZA WEWE MWENYEWE,
(usiwe unaomba ushauri sana kuhusu maisha yako fanya moyo unavyokutuma)
10.USIWAHUKUMU WATU KABLA HATA HUJAWAJUA
(usipende kufikiria ubaya kwa kumtazama tu mtu sura yake)
11.SHUKURU KWA ULICHONACHO,USIJUTIE KILE AMBACHO HUNA
(usipokifurahia wakati unacho,kitakapopotea utaanza kukikumbuka na kujuta kwa nini hujakithamini)
12.FURAHIA MAFANIKIO YA WENZAKO,USIONE AIBU KUSIFU KISICHO CHAKO
(ufate moyo wako kwa kusifu kila kilicho kizuri,hata kama si chako)
13.UKIFURAHISHWA NA KITU WAAMBIE NA WENZAKO,USIFURAHIE PEKE YAKO
(kua na kampan ni bora zaidi ya kukaa peke yako)
14.USIMSHAWISH MWENZAKO ABADILIKE ALIVYO,KWANI ALIVYO NDIVYO ALIVYO
(utakapotaka kumbadili,akigoma mnaweza kua maadui,bora muache kama alivyo)
15.UKIWA SAFARINI FURAHIA SAFARI,SI KUWAZA UTAFIKA SAA NGAPI
(ukiwaza sana unaweza kuanza kuona gari haiendi kasi sana na baadae ukaja juta kwa haraka zako)
16.JIZUIE KUWAZA MAMBO MABAYA,JILAZIMISHE KUWAZA MAZURI
(kwani unavyowaza mabaya kila muda mwisho utakuja kutenda maovu)
17.ELEWA FURAHA NI JAMBO KUBWA SANA MAISHANI KULIKO HATA UTAJIRI
 (ridhika na furahia na kila jambo lako ulilofanikisha,japo ni kidogo
18.TUMIA NGUVU ZAKO KWA UMAKINI,
(usitumie kwa kufanya mambo ya kijinga.usisikitike,usijute na wala kunung’unika,,,)
19.KUA JASIRI KAMA KUNA KITU CHA KUBADILI KIBADILI MARA MOJA USISITE
(Usisite kufanya maamuzi kwani unaweza kuwaza jambo jingine likavuruga wazo zuri la mwanzo)
20.FURAHIA KAZI YAKO
(jali na kuiona kazi yako unayofanya ni bora kuliko kitu chochote)
21.USIKATE TAMAA,MATATIZO YAKO YAFANYE YAWE NI CHANGAMOTO YA KUPIGANA ZAIDI
(matatizo hayakimbiwi,yanatatuliwa)
22.TAFUTA NJIA TOFAUTI TOFAUTI ZA KUTATUA MATATIZO YAKO,
(usilazimishe njia moja,jaribu kutafuta suluhisho jingine kama unalotumia unaona halisaidii)
23.KUA HURU UKIAMINI KILA MTU YUKO HURU
(fanya jambo kwa maamuzi yako si ya kuambiwa)
24.TANUA MAWAZO KWA KUWAZA VITU TOFAUTI TOFAUTI
(usiwaze kitu hicho hicho kila siku,ukikiwaza kitu kimoja unaweza kupata wazimu)
25.USISUMBUKE NA WATU UNAOONA NI WABISHI KWA KILE ULICHO NA UHAKIKA NACHO
(chunguza wa kuwaelewesha,kuna wengine wamezaliwa wabishi)
26.KUA MKWELI KWA NAFSI YAKO NA KWA WENZAKO
(ukiurudia rudia uongo mwisho unakukaa mawazoni hadi mwenyewe unaamini ni ukweli)
27.JIKUBALI ULIVYO,KWANI ULIVYO NDIVYO ULIVYO
(ulivyo ndivyo ulivyo,na alivyo mwingine ndivyo alivyo)
28.HESHIMU KILA MTU,USIMDHARAU YEYOTE
(fikiria sana kabla ya kumdharau mtu,ingekua wewe umedharauliwa ingekuaje?)
29.ISHI SASA USIWAZE BAADAE ITATOKEA NINI
(usiogope sana kuhusu baadae,utakua huna amani maisha yote)
30.USIAHIRISHE JAMBO FANYA KWA MUDA
(mwisho wa kuahirisha ni kutokufanya kabisa)

31.USIWEKE VISASI,SAMEHE MARA MOJA NA UENDELEE NA MAISHA,
(ukiweka sana visasi,hutafanya mambo yako kwa amani lakini ukisamehe utakua huru daima)

32.MALIZA TATIZO,USISITE AU KUWAZA MBELE ITAKUAJE
(mwisho wa tatizo ni furaha)
33.KAA NA WATU WATAKAOKUPA FURAHA SI MAUDHI
(usikae na watu wanaotengeneza majungu na fitna)
35.JITETEE MWENYEWE
 (hakuna wa kupigana vita yako),,,,
36.JIPENDE
   ( ukijpenda na watu watakupenda)
37.FANYA KITU UNACHOPENDA,USIJINYIME
(usiige wanavyofanya watu ili na wewe uonekane mjanja,fanya unalomudu)
38.ANDIKA MAWAZO NA MALENGO YAKO
(na uvifanye hatua kwa hatua na usikate tamaa kama mambo hayaendi vizuri)
39.FANYA VITU VITAKAVYOKUPA FURAHA
(jitahidi kutoa msaada kila unapoweza)
40.KILA MARA JITAHIDI KUSONGA MBELE,
(usiwe unajikumbusha sana mambo yaliopita…..)

    INGAWA NI LISTI NDEFU LAKINI INA MANUFAA SANA,JARIBU KUCHAGUA MAMBO 18 HALAFU YAFANYIE KAZI NINA UHAKIKA UTAISHI KWA FURAHA NA AMANI SANA…

No comments:

Post a Comment